Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini (Chadema), Mchungaji Peter
Msigwa na mbunge wa Iramba Magharibi (CCM), Mwigulu Nchemba jana nusura
wachapane makonde baada ya kutupiana maneno ya kashfa, wakituhumiana
kuhusika na mlipuko wa bomu uliotokea Jumamosi iliyopita mkoani Arusha.
Tukio hilo lilitokea katika viwanja vya Hoteli ya
St Gasper nje kidogo ya mji wa Dodoma, walipokwenda kwa ajili ya
kuhudhuria semina ya wabunge wapambanaji na Ukimwi, ambapo baadhi ya
wabunge wa Chadema walihudhuria, baada ya kutoonekana mjini humo tangu
Juni 17 mwaka huu.
Wabunge hao wa Chadema hawakuhudhuria kikao
chochote cha Bunge kutokana na kwenda mkoani Arusha kwa shughuli
mbalimbali, kutokana na mlipuko wa bomu uliotokea katika mkutano wao wa
kuhitimisha kampeni zake za uchaguzi mdogo wa udiwani katika viwanja vya
Soweto, Juni 16 jijini humo.
Malumbano hayo yanatokana na Nchemba kuituhumu
Chadema kuhusika na mlipuko huo, Juni 20 mwaka huu wakati akichangia
hotuba ya Bajeti Kuu ya Serikali ya mwaka 2013/2014, akisema chama hicho
kilipanga kulipua bomu hilo ili kuwafanya Watanzania waamini kuwa
Serikali ya CCM ndiyo inayohusika na tukio hilo.
Chanzo gazeti la mwananchi.
Chanzo gazeti la mwananchi.
Post a Comment