Social Icons

Loading...

Simba Yaicharaza Azam FC 3 - 2 , Yatwaa Ngao ya HISANI

Ngao ya Hisani iliyotwaliwa na Simba Sports Club kuzindua msimu wa ligi ya 2012/2013
Nahodha na golikipa namba moja wa Simba Juma Kaseja akinyanyua juu ngao ya hisani

Nahodha wa klabu ya Simba Juma Kaseja Juma anapokea ngao ya hisani kwa mwaka wa pili mfululizo; anapokea ngao ya hisani ya kufungua pazia la msimu wa mwaka 2012/2013 toka kwa Naibu waziri wa Kazi, vijana na michezo Mhe. Makongoro Mahanga.

Baada ya Azam kutangulia kwa "baiskeli ya miti" kwa magoli ya Kipre Tchetche na John Bocco “Adebayor” Simba ilikuja kwa kasi na uzito wa kiberenge na kusawazisha magoli hayo na kuongeza lingine kupitia kwa Daniel Akuffor (penati), Emmanuel Okwi na Mwinyi Kazimoto. Simba imeshinda mabao 3 kwa 2 ya Azam FC.

Azam FC wanalia hasa Salum Abubakar kwa kushindwa kutwaa ngao hii. Shomari Kapombe anaibuka mchezaji bora wa mechi ya leo, ingawa Emmanuel Okwi na Mrisho Ngasa walimeikimbiza mno ngome ya Azam FC. Pamoja na ushindi huu kocha wa Simba Mirovan nCircovic ana kibarua kizito kuisuka ngome yake ya ulinzi kwani bado haijatulia.


Ushindi huu wa pili mfululizo unamaanisha kuwa ikiwa klabu ya Simba itanyakua tena ngao hiyo katika msimu ujao itakuwa imeitwaa ngao hiyo ya hisani jumla/moja kwa moja na hivyo kuandika historia mpya nchini. Simba ndio pia walikuwa wa kwanza kunyakua ngao hiyo tangu mfumo huu ulivyoanza nchini.

Kwa ushindi huu unaifanya klabu ya Simba mpaka sasa kuwa imejikusanyia makombe manne (4) katika mwaka huu wa 2012; makombe mengine ni kombe la ligi kuu ya Tanzania Bara "Vodacom Premier League", Kombe la Urafiki na kombe la mashindano ya muungano.

Pamoja na ushindi huu kocha wa Simba bado ana kibarua kizito kurekebisha mapungufu lukuki katika safu yake ya ulinzi hasa mabeki wa kati na pia kwenye nafasi ya ushambuliaji kwani wachezaji wake wanapoteza nafasi nyingi sana za kufunga magoli.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top