Social Icons

Loading...

Sauti za wananchi wa Dar kuhusu tatizo la foleni

Kwa wakazi wa Dar es Salaam, moja ya kero kubwa ni kukithiri kwa foleni za magari barabarani.
Hakuna asiyeguswa na atizo hilo kutokana na ubovu wa miundombinu na kutokuwepo na miundombinu ya kisasa ya usafiri ikilinganishwa na ongezeko la watu.
Ni mkoa unaoongoza kwa watu kupoteza muda mwingi barabarani, kiasi cha kuzorotesha hata utendaji wa kila siku na kuathiri shughuli za uchumi ambazo ni muhimu kwa maendeleo ya nchi.
Tatizo hili la foleni linaelezewa na wataalamu kwamba husabisha matatizo mbalimbali ya kiafya, ikiwa ni pamoja na watu kupatwa na ugonjwa wa kurukwa akili. Kisa cha haya yote ni foleni hizo ambazo inaonekana wazi kuwa zimekosa mwarobaini wa uhakika.
Hata hivyo, kama sehemu mojawapo ya kukabiliana na tatizo hilo, Serikali inaendelea na mradi wa mabasi yaendayo kasi. Kukamilika kwa mradi huo kunaelezwa kuwa kutasaidia kwa kiasi kupunguza tatizo la foleni barabarani katika baadhi ya maeneo ambayo mradi huo umeyagusa.
Hata hivyo, baadhi ya wakosoaji wanasema kuwa kuwapo kwa mradi huo wa mabasi yaendayo kasi hakuwezi kusaidia moja kwa moja kuondoa tatizo hilo ambalo limeendelea kuongezeka kutokana na ongezeko kubwa la idadi ya watu na kupanuka kwa shughuli za kiuchumi.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top