Rais Jakaya Kikwete amevitaka vyuo vikuu nchini kuweka nguvu
zaidi, kuhakikisha vinadahili wanafunzi wa shahada za juu ili kupata
wahadhiri.
Akizungumza baada ya kutoa hati idhini kwa Vyuo
Vikuu na Vyuo Vikuu Vishiriki vinane, Rais Kikwete alisema kufanya hivyo
vitakabiliana na tatizo la uhaba wa wahadhiri linalovikabili hivi sasa.
“Pale kwenye upungufu tusisite kutafuta wataalamu
wengine kutoka nje ya nchi. Wakati wa miaka ya 1970 tulipokuwa tunasoma
pale Chuo Kikuu (Mlimani), tulikuwa na wahadhiri wengi kutoka nje,”
alisema Rais Kikwete.Licha ya suala hilo, Rais Kikwete alisisitiza umuhimu wa vyuo hivyo kuwekeza kwenye utoaji elimu bora.“Ikumbukwe idadi kubwa ya wanafunzi haitoshi,
lazima tuzingatie ubora. Tunataka mwanafunzi anayepata shahada nchini
ajulikane popote anapokwenda,” alisema Rais Kikwete na kuongeza
Taarifa kwa hisani ya mwananchi.
Taarifa kwa hisani ya mwananchi.
Post a Comment