Social Icons

Loading...

CAG apewa maagizo ya kukagua ufisadi wa bil 13.

Kamati ya Kudumu ya Hesabu za Serikali Kuu (PAC), imeiagiza ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG) kufanya ukaguzi maalumu wa matumizi ya Sh13 bilioni, katika Mkutano wa Benki ya Maendeleo Afrika (ADB) uliofanyika Mei mwaka 2012.
Uamuzi huo umekuja baada ya kubainika kwa matumizi mabaya ya fedha hizo, yaliyofanywa na Hazina kwa ajili ya ununuzi wa samani za ofisini na kompyuta ndogo 200.
Mwenyekiti wa kamati hiyo, Zitto Kabwe alisema mbali na vituo hivyo, Hazina pia imenunua, seti za televisheni za ukutani, mashine za kuchapishia karatasi, viti na makochi ya sebuleni.
Alisema ingawa vifaa hivyo vimenunuliwa kwa fedha za Serikali, baadhi yake vimeachwa katika ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha, bila ya kuwapo kwa makabidhiano ya kisheria.
“Kamati imepata mashaka kuhusu matumizi ya Sh13 bilioni katika mkutano wa ADB, jambo lililotufanya tumuombe CAG kufanya ukaguzi maalumu wa matumizi ya fedha hizi za Serikali,” alisema Zitto.
zaidi  soma 
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top