Mtangazaji wa idhaa ya kiswahili BBC Ndg Salim Kikeke. |
Licha ya kauli hii ya Dk Dyneer, kuna vijana wengi
nchini wanaonekana wamekata tamaa; Wengine hufikiri kwamba kama
umezaliwa katika familia duni, maana yake utakuwa na maisha duni milele,
huku wale ambao wamezaliwa katika familia tajiri, wanafikiri
wataendelea kuwa tajiri.Hata hivyo ukweli ni kwamba mtu yeyote anaweza
kuwa na maisha bora, kama anavyosema msomi Hope Clark katika kitabu
chake Fedha za Waandishi cha hivi karibuni nchini Ireland, kwamba siri
ya kufanikiwa katika maisha ni kuishi kwa malengo, kuishi vizuri na watu
na kupenda kuwa karibu na wasiokata tamaa.
Mwalimu Julius Nyerere wakati fulani amewahi
kunukuliwa akisema ‘Uchumi mnao, mmeukalia’. Kila mtu alitafsiri
alivyoweza, lakini ukweli hasa ni kwamba mtu yeyote akijipanga vizuri
kwa maana ya kutuliza akili yake, kukaa na watu wa kumshauri vizuri na
kufanyia kazi mambo au mipango anayoipanga, anaweza kufanikiwa
anachotaka...Ni ukweli kuwa kuna wengi wana maisha duni kwa sababu
pamoja na mambo mengine ya tabia zao za kukata tamaa, waoga wa
kuthubutu.
Kati ya vijana ambao wanaonekana kupambana hadi
kuweza kujenga majina na heshima zao Duniani ni Salim Kikeke; Ni mtu
ambaye kama angekata tamaa hakika asingefika aliko sasa.
Sasa amekuwa ni mtu wa kujadiliwa na umaarufu wake
hauko tu Tanzania, bali maeneo mengi ya Dunia hasa kunakozungumzwa
Kiswahili. Huyu mtu ni kati ya watangazaji wakongwe na kivutio cha watu
wengi kutoka barani Afrika na duniani kote, lakini katokea wapi?
Taarifa kamili bofya kikeke
Taarifa kamili bofya kikeke
Post a Comment