Social Icons

Loading...

FAHAMU Salim Kikeke wa BBC wapi kapitia hadi kufika pale alipo.

Mtangazaji  wa  idhaa ya kiswahili BBC  Ndg Salim Kikeke.
Penye nia pana njia na mtafutaji makini huwa hachoki, ndivyo anavyosema mtaalamu wa masuala ya uchumi, Dk Wayne Dyer wa Marekani katika kitabu chake cha ufanye nini kupata unachokiazimia.
Licha ya kauli hii ya Dk Dyneer, kuna vijana wengi nchini wanaonekana wamekata tamaa; Wengine hufikiri kwamba kama umezaliwa katika familia duni, maana yake utakuwa na maisha duni milele, huku wale ambao wamezaliwa katika familia tajiri, wanafikiri wataendelea kuwa tajiri.Hata hivyo ukweli ni kwamba mtu yeyote anaweza kuwa na maisha bora, kama anavyosema msomi Hope Clark katika kitabu chake Fedha za Waandishi cha hivi karibuni nchini Ireland, kwamba siri ya kufanikiwa katika maisha ni kuishi kwa malengo, kuishi vizuri na watu na kupenda kuwa karibu na wasiokata tamaa.
Mwalimu Julius Nyerere wakati fulani amewahi kunukuliwa akisema  ‘Uchumi mnao, mmeukalia’. Kila mtu alitafsiri alivyoweza, lakini ukweli hasa ni kwamba mtu yeyote akijipanga vizuri kwa maana ya kutuliza akili yake, kukaa na watu wa kumshauri vizuri na kufanyia kazi mambo au mipango anayoipanga, anaweza kufanikiwa anachotaka...Ni ukweli kuwa kuna wengi wana maisha duni kwa sababu pamoja na mambo mengine ya tabia zao za kukata tamaa, waoga wa kuthubutu.

Kati ya vijana ambao wanaonekana kupambana hadi kuweza kujenga majina na heshima zao Duniani ni Salim Kikeke; Ni mtu ambaye kama angekata tamaa hakika asingefika aliko sasa.
Sasa amekuwa ni mtu wa kujadiliwa na umaarufu wake hauko tu Tanzania, bali maeneo mengi ya Dunia hasa kunakozungumzwa Kiswahili. Huyu mtu ni kati ya watangazaji wakongwe na kivutio cha watu wengi kutoka barani Afrika na duniani kote, lakini katokea wapi?
Taarifa  kamili   bofya   kikeke  
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top