Social Icons

Loading...

AMBAVYO WENGER HATOMSAHAU DROGBA ALIYEKATAA KUMSAINI KWA PAUNI 100,00 TU AKIWA KINDA TENA UFARANSA

KAMA Arsene Wenger alihitaji ukumbusho wowote wa kosa alilofanya katika usajili akiwa kazini Arsenal, Didier Drogba alifanya hivyo Uwanja wa Emirates Jumapili.
Mabao mawili ya Drogba ya dakika za lala salama dhidi ya Arsenal yaliyowezesha Galatasaray kubeba Kombe la Emirates yameendeleza rekodi ya mshambuliaji huyo dhidi ya The Gunners na kufika mabao 15 katika mechi 15.
Kwamba, katika dakika 1175 ambazo Drogba amecheza dhidi ya Arsenal, amefunga wastani wa bao moja katika kila dakika 78 na sekunde 20.
Ulikuwa usiku wa pigo kwa Wenger, ambaye alikataa kumsajili Drogba kwa Pauni 100,000.
Akiwa anachipukia nyota huyo wa Ivory Coast katika miaka yake minne Le Mans kati ya mwaka 1998 na 2002, jicho la skauti wa Wenger lilimnasa mchezaji huyo.
Wenger alikataa kumsajili, na Drogba akahamia timu nyingine ya Ligue 1, Guingamp akiwa ana umri wa miaka 23 kwa Pauni 80,000.
Wenger alisema mwaka 2009: "Tumemuangalia kwa umakini alipokuwa Le Mans. Siyo sisi tu tuliomuangalia. Lakini tulifikiri hawezi tayari kiasi cha kutosha. "Lilikuwa ni kosa, lakini ukiwa kwenye soka, kila mmoja anaweza kuelewa. Tulikuwa na Thierry Henry. Tulisema tutafuatilia maendeleo ya Drogba. Hatukuwahi kumkataa,"
Mwaka 2004, kufuatia msimu wa mafanikio makubwa akiwa Marseille, Drogba alisaini Chelsea kwa ada ya Pauni Milioni 24.
Kana kwamba hilo halikuwa pigo tosha katika jino la Wenger, Drogba aliifanyizia ile mbaya timu yake uwanjani.Alifunga mabao 13 katika mechi 14 dhidi ya Arsenal enzi zake akiwa Stamford Bridge, mengi kati yao akifunga katika mechi muhimu.
Wenger alipata ahueni wakati Drogba alipoondoka Chelsea kuhamia Shanghai Shenhua mwaka jana, akisema wakati huo: "Sijui ni kiasi gani Chelsea wamempoteza, lakini hatumkumbuki. Amefanya madhara mengi dhidi yetu katika kila mechi,".
Drogba anaweza kuwa ukingoni mwa soka yake akiwa na umri wa miaka 35 sasa, lakini kwa Emirates atabakia kukumbukwa kama kiboko ya timu ya Wenger hadi siku atakapotungika daluga zake.
Mfaransa huyo sasa atakuwa anaomba dua Arsenal isipagwe kundi moja na Galatasaray katika Ligi ya Mabingwa katika droo inayotarajiwa kupangwa mjini Monaco Agosti 29.
Taarifa  na  picha  kwa   hisani  ya bin Zubeiry.   
 
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top