Social Icons

Loading...

Walinzi wa amani Darfur wadaiwa hawana zana za kisasa .

Katibu Mkuu Mstaafu wa Umoja wa Nchi Huru za Afrika (OAU), Dk Salim Ahmed Salim, amesema umahiri wa vikosi vya kulinda amani Darfur na kwingine Afrika unatia shaka, kwani vinakabiliwa na upungufu wa vitendea kazi ikiwamo zana za kisasa.
Kauli ya Dk Salim inakuja ikiwa ni siku chache baada ya kuuawa kwa wanajeshi saba wa Tanzania waliokuwa wakitumikia Vikosi vya Kulinda Amani vya Umoja wa Mataifa na Afrika (Unamid).
Wanajeshi hao waliuawa wakiwa katika majukumu yao na kundi la Wanamgambo, linalodaiwa kuiunga mkono Serikali ya Rais Said al-Bashar la Janjaweed.
Dk Salim alisema himizo la kutaka kubadilishwa kwa kifungu cha sita kwenda saba, liende sanjari na zana za kisasa ambazo waasi hao wanatumia ikilinganishwa na walinzi wa amani wanaotumia silaha za kawaida.
Chanzo:http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/Walinzi-wa-amani-Darfur-wadaiwa-/-/1597296/1925656/-/cgb97e/-/index.html
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top