Waziri
wa Fedha Dk. William Mgimwa akisisitiza jambo juu ya tozo la kodi
katika laini za simu wakati alipokutana na waandishi wa habari leo
jijini Dar es Salaam.Serikali yawataka wananchi kutokuwa na wasiwasi kuhusiana na mpango wa ukusanyaji wa kodi ya laini za simu.
Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa
Fedha Dk. William Mgimwa alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari
jana jijini Dar es Salaam.
Mgimwa amesema kuwa Serikali
inaendelea kukutana na wadau mbalimbali ili kujadili na kupokea
mapendekezo kuhusiana na dhamira ya Serikali kutoza kodi kutoka katika
laini za simu.
Aliongeza kuwa Serikali ina nia
njema ya kuongeza mapato yake ili kuongeza kasi ya kutoa huduma za
msingi kwa wananchi wake hususani wa vijijini.
“Lengo hasa la kodi hii ni kuboresha
huduma za msingi vijijini kama umeme, maji na barabara ambazo ni duni
sana vijijini, hata hivyo tunafanyia kazi mapendekezo mbalimbali ya
wananchi na wadau wenye mitazamo mbalimbali” alisema Dk. Mgimwa.
Aidha Dk. Mgimwa amesema kuwa hivi
karibuni amekutana na chombo cha watoa huduma za mawasiliano (MoAT)
nakujadiliana nao na kuwaahidi kuwa mapendekezo yao yatafanyiwa kazi.
Mkutano huo umekuja baada ya wadau
mbalimbali kutoa malalamiko juu ya uwepo wa tozo ya kodi ya laini za
simu ambapo mmiliki wa laini ya simu atatakiwa kulipia shilimgi 1000
kila mwezi mara kodi hiyo itakapo anza kutozwa.
Picha na Frank Shija – Maelezo
Post a Comment