Social Icons

Loading...

KUELEKEA UCHAGUZI 2015.

HUKU Chama Cha Mapinduzi (CCM), kikiwa kimeweka bayana kwamba hakiungi mkono Serikali tatu kama Rasimu ya Katiba inavyoonyesha, Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe ameibuka na kusema endapo Mabaraza ya Katiba yatawasilisha hoja za kuikubali, kuna uwezekano mkubwa wa Uchaguzi Mkuu wa 2015 kukwama.
“Uwepo wa Serikali tatu utafumua mfumo mzima wa utendaji ndani ya Serikali. Hatuwezi tena kufanya uchaguzi wa Rais na wabunge 2015, hatuwezi kufanya chochote nje ya Katiba ya Serikali Tatu kwa kuwa kinachofuata ni kuunda Katiba nyingine inayohusiana na Serikali tatu.“Kama tutafanya uchaguzi, utafanyika kwa taratibu zipi, ipi itakuwa mipaka ya marais wa Serikali tatu, makamu na mawaziri wakuu, mfumo wa Mahakama, Tume ya Uchaguzi, utendaji wa Bunge na wabunge, yako mengi, sasa mpaka hayo yaingie kwenye Katiba,” alisema Chikawe juzi Dar es Salaam.
Alisema lazima CCM isimamie suala hilo kwa kuwa kukubali Serikali tatu kutaua Muungano ambao sehemu kubwa unalindwa na chama hicho tawala.
“CCM wamejipanga kama baraza na kusimamia hili la Serikali mbili ambalo lengo ni kuulinda Muungano. Litakapokuja hili la Serikali tatu, lazima Muungano uparaganyike,” alisema.Hata hivyo, kauli hiyo ya Waziri Chikawe inakinzana na ile aliyoitoa Juni 4, siku moja baada ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba kutangaza hadharani Rasimu hiyo.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top