Social Icons

Loading...

Mabomba ya kusafirisha gesi yatua Mtwara.

Meli kubwa kutoka China tayari imetua katika Bandari ya Mtwara kwa ajili ya kushusha mizigo ya mabomba ya gesi ili kuanza kwa kazi ya ujenzi wa bomba la kusafirisha gesi kutoka Mtwara kwenda Dar es Salaam.Mmoja wa watumishi ndani ya Bandari ya Mtwara ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini, alisema zaidi ya magari 20 yanatakiwa kupakua mzigo wa mabomba zaidi ya 4,000 kutoka bandarini hapo na kusafirishwa kwenda Kiranjeranje Lindi kwa ajili ya zoezi zima la ujenzi wa bomba hilo.
“Hayo magari mliyoyaona ni miongoni mwa zaidi ya magari 20 yanayokuja kupakua mzigo wa mabomba ambayo ni zaidiya 4,000 kwa ajili ya kuyapeleka maeneo mbalimbali ikiwemo Kiranjeranje Lindi kwa ajili ya kufanikisha zoezi la ujenzi wa njia ya kusafirisha gesi, upakiaji unaendelea hapa Mtwara na Dar meli inapakuwa mzigo ili kupelekwa kwenye maeneo husika na upakuaji kwa mikoa yote unaendelea kwa amani,” alisema.Akizungumza na gazeti hili mmoja wa madereva wa magari maalumu kwa ajili ya kupakua mzigo wa mabomba,alisema wametokea Dar es Salaam na hii ni zabuni maalumu waliyoipata kwa ajili ya maandalizi ya kupokea mizigo na kupeleka yanakotakiwa hapo baadaye baadaye baada ya kukabidhiwa kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda.
Chanzo : http://www.mwananchi.co.tz/-/1597570/1916578/-/104vy0r/-/index.html
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top