Social Icons

Loading...

Mwalimu ajifungua watoto 5 kwa mpigo, waishi kwa saa kumi na kufariki dunia .

MWALIMU Sophia Mgaya(28) mkazi wa Ruhuwiko mjini Songea mkoani Ruvuma aliyejifungua watoto watano kwa wakati mmoja kwa njia ya upasuaji mnamo Mei 25 mwaka huu katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Ruvuma iliyopo mjini Songea na watoto hao kuishi kwa muda wa masaa kumi kabla hawajafariki dunia ameruhusiwa kutoka hospitalini hapo.
Akizungumza na Demashonews kwa njia ya simu Sophia Mgaya akiwa nyumbani kwake Ruhuwiko mjini Songea alisema alilazimika kuomba kutoka wodini kwa sababu alikuwa akijisikia uchungu anapowaona wanawake wenzake wodini humo wakiwakumbatia watoto wao baada ya kujifungua huku wa kwake wote wakiwa wamefariki dunia baada ya kuzaliwa. 
           Alisema kuwa muda wote aliokuwa hospitalini hapo baada ya watoto wake kufariki huku akiwa bado anauguza kidonda cha upasuaji aliofanyiwa alikuwa akilia muda wote anapowaona wanawake wenzake waliojifungua wakiwakumbatia na kuwanyonyesha watoto wao hivyo akaamua kuomba aruhusiwe kutoka hospitalini hapo. 
 ‘’Niliomba kuruhusiwa kutoka hospitali na kwenda kujiuguza kidonda nyumbani kwa sababu ya uchungu na majonzi niiiyokuwa nikiyapata wodini hapo ninapowaona wanawake wenzangu waliojifungua wakiwakumbatia na kuwanyonyesha watoto wao huku wa kwangu wakiwa wameshazikwa”alisema Bi.Mgaya
Chanzo :  http://www.jukwaahuru.com/?p=16011
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top