Social Icons

Loading...

Mwananchi yazoa tuzo za umahiri

Waandishi wa Kampuni ya Mwananchi Communications Limited (MCL) inayochapa magazeti ya Mwananchi, The Citizen na Mwanaspoti wameibuka tena kidedea kwenye tuzo  za umahiri wa Uandishi wa Habari Tanzania (EJAT) kwa mwaka 2012, baada ya kushinda tuzo 13, ikiwamo ya mshindi wa jumla.
Sherehe za utoaji wa tuzo hizo ilifanyika jana katika Ukumbi wa Diamond Jubilee na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwamo Makamu wa Kwanza wa Rais, Seif Sharif Hamad ambaye alimwakilisha Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein.
Mshindi wa jumla kwa mwaka 2012 ni Lucas Liganga wa gazeti la The Citizen, ambaye ameifanya MCL kunyakua tuzo hiyo kwa miaka miwili mfululizo ambapo mwaka 2011 tuzo hiyo ilichukuliwa na Neville Meena wa gazeti la Mwananchi.
Washindi walipewa zawadi za magodoro, televisheni, Ipad na vyeti, huku mshindi wa jumla akipewa dola 4,000 za kujiendeleza kimasomo.
MCL iliingiza fainali waandishi 14 kati ya 66 walioteuliwa kuwania tuzo hizo ambao ni pamoja na Samweli Mwamkinga, Florence Majani, Polycarp Machira, Tom Musoba, Elias Msuya, Leon Bahati, Lucas Liganga, Shija Felician, Fredy Azzah, Joseph Zablon, Zephania Ubwani, Tumaini Msowoya, Anthony Mayunga na Edward Qorro.
Mbali na kutoa mshindi wa jumla, waandishi sita wa magazeti hayo walikuwa ndio wagombea pekee wa tuzo mbili za habari bora ya Uchumi na Biashara na Majanga, huku Azzah akishinda tuzo ya habari bora ya Virusi vya Ukimwi (VVU) ambapo alikuwa peke yake na alichaguliwa mara mbili kuwania tuzo hiyo.
Waandishi wa MCL walioshinda na tuzo zao katika mabano ni Edward Qorro (Uchumi na Biashara), Lucas Liganga (Mazingira na Malaria), Fredy Azzah (Ukimwi na Elimu), Anthony Mayunga (Utawala Bora).
Wengine ni Florence Majani (Sayansi na Teknolojia na Afya ya Uzazi), Samwel Mwakibinga (Mchora katuni bora), Zephania Ubwani (Kilimo), Polycarp Machira (Majanga), Shija Felician (Tuzo ya wazi).
Katika tuzo ya jumla MCL iliingiza waandishi watatu kati ya waandishi wanane waliochaguliwa kuwania tuzo hizo ambao ni Lucas Liganga, Fredy Azzah na Florence Majani.
Katika utoaji wa tuzo hizo, MCL ilifuatiwa na Shirika la Utangazaji (TBC) ambalo lilizoa tuzo nane, Afya Redio (6) na Kilimanjaro Film Institute (5).
Chanzo: gazeti  la  mwananchi
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top