ALIYEKUWA Mwenyekiti wa Kamati ya
Usajili ya Simba SC na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji, Zacharia Hans
Poppe, ameamua kujiuzulu nyadhifa zote hizo kwa sababu
kuna mgawanyiko ndani ya uongozi unaokwamisha maendeleo.
“Ni wazi kuwa kwenye uongozi tumekuwa
hatufanyi kazi kwa umoja na mgawanyiko huu unatukwaza na hatuwezi kupata
maendeleo,”alisema Hans Poppe.
“Baada ya kutafakari, nimeona ni bora
nijiuzulu nyadhifa hizo kupisha wengine ambao wanaweza wakawa na mawazo
mapya ya kuendeleza klabu, nami nitabakia kuwa mwanachama mwaminifu
daima,”alisema Hans Poppe.
Poppe amewasilisha barua ya kujiuzulu
Simba SC jana na wazi kujiuzulu kwa Kapteni huyo wa zamani wa Jeshi la
Wananchi Tanzania (JWTZ) ni pigo kwa klabu hiyo, kwani alikuwa
akiisaidia mno kwa hali na mali.Aidha, kujiuzulu kwa Hans Poppe wazi
kutachochea zaidi mgogoro ndani ya klabu hiyo na kuongeza shinikizo la
viongozi wa klabu hiyo kujiuzulu pia.
Simba SC kwa sasa haifanyi vizuri katika
Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara na tayari imekwishatolewa katika Ligi
ya Mabingwa Afrika baada ya kufungwa jumla ya mabao 5-0 na Recreativo
de Libolo ya Angola katika raundi ya kwanza tu.
Ubingwa wa Ligi Kuu ni kama umekwishaota mbawa, kwani hadi sasa
Wekundu hao wa Msimbazi wanashika nafasi ya tatu wakiwa na pointi 31,
sawa na Coastal Union ya Tanga na Mtibwa Sugar ya Morogoro, nyuma ya
Azam FC yenye pointi 36 na Yanga inayoongoza kwa pointi zake 42, zote za
Dar es Salaam.
Godfrey Nyange naye ajiuzulu kwa e-mail
MAKAMU Mwenyekiti wa Simba SC, Geoffrey
Nyange ‘Kaburu’ inadaiwa amemuandikia barua pepe, Mwenyekiti wa klabu
hiyo, Alhaj Ismail Aden Rage kumtaarifu kujiuzulu wadhifa huo.Kaburu anakuwa kiongozi wa pili wa
Kamati ya Utendaji ya Simba kujiuzulu , baada ya awali mchana,
Zacharia Hans Poppe aliyekuwa Mjumbe kujiuzulu pia.
Hans Poppe, aliyekuwa pia Mjumbe wa
Kamati ya Utendaji, alisema kwamba ameamua kujiuzulu nyadhifa zote hizo
kwa sababu kuna mgawanyiko ndani ya uongozi unaokwamisha maendeleo.
Chanzo : Bin Zubeiry Blog.
Post a Comment