Social Icons

Loading...

Hoja ya Mbatia kuhusu Elimu Yazimwa Bungeni

HOJA binafsi ya mbunge wa kuteuliwa, James Mbatia, imeibua mapya bungeni mjini Dodoma, baada ya Kambi ya Upinzani kukutana kwa dharura, kupinga kufifishwa hoja hiyo na Naibu Spika, Job Ndugai, wakidai anataka kuizima.Juzi Mbatia aliwasilisha bungeni Hoja Binafsi kuhusu udhaifu wa elimu Tanzania, akitaka mfumo mzima unaosimamia elimu nchini ufumuliwe.Baada ya majadiliano marefu kuhusu kuundwa kwa kamati ya kuchunguza mitalaa, sera namihutasari ya elimu, hoja mbalimbali zilitolewa, baadhi ya wabunge wakitaka Kamati ya Bunge, huku wengine wakitaka iundwe tume huru ya kufuatilia suala hilo.Mjadala huo uliendelea jana asubuhi kwa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa kusimama na kutetea mfumo wa elimu uliopo na mtalaa, kabla ya wabunge kuchangia na Mbatia kuhitimisha.

Akiwasilisha hoja yake, Mbatia aling’ang’ania kupatiwa mtalaa wa masomo ya elimu kwa shule za msingi na sekondari, jambo ambalo, Waziri Kawamba alijibu kuwa ulikuwapo ingawa hakuwa nao bungeni.
Baada ya majibu ya Dk Kawambwa, Mbatia aliomba hoja yake iahirishwe hadi mtalaa utakapowasilishwa bungeni.Awali, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge, William Lukuvi alisimama na kusema akihoji: “Katika kikao kilichopita, hata katika Hansard, tulisema mtalaa utawasilishwa katika kikao hiki, sasa wasiwasi wa mbunge (Mbatia) ni nini? Hata siku ya mwisho ya Bunge tutaleta.”

Baada ya kauli hiyo, Naibu Spika, Job Ndugai alipiga kura kwa kuuliza wanaotaka hoja imalizike na baada ya majibu, aliruhusu Mbunge wa Nzega, Dk Hamis Kigwangalla kuwasilisha Hoja Binafsi kuhusu ajira kwa vijana na kilimo.Hata hivyo, baada ya kumruhusu Dk Kigwangalla, wabunge wa upinzani walitoka nje ya Bunge na kufanya mkutano wa dharura uliochukua dakika 38 katika Ukumbi wa Pius Msekwa.
Soma  zaidi :  http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/-/1597296/1682392/-/11s9j2s/-/index.html
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

1 comments:

Safi sana mheshimiwa Mbatia,Mungu akubariki.

Reply

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top