Social Icons

Loading...

UTAFITI: Watoto wa kike wanaelewa haraka darasani kuliko wa kiume

UTAFITI mpya wa masuala ya elimu umebainisha kwamba wanafunzi wa kike hufanya vizuri zaidi darasani kuliko wanafunzi wa kiume.
Matokeo ya utafiti huo, uliofanywa hivi karibuni na wataalamu wa elimu kutoka vyuo vikuu vya Georgia na Columbia vya nchini Marekani, umebaini kuwa watoto wa kike wa kati ya umri wa miaka sita hadi 12, huelewa kwa haraka darasani kuliko watoto wale wa  kiume.
Wameeleza kuwa wanafunzi hao wa kike huwa makini zaidi kumsikiliza mwalimu anapokuwa akifundisha darasani, tofauti na watoto wa kiume, ambao hutumia muda mwingi kufanya mambo mengine ikiwamo kucheza, kuchokozana na pengine kugombana wao kwa wao.
Matokeo hayo yaliyochapishwa katika Jarida la Rasilimali Watu la Marekani na kuandikwa kwenye mtandao wa Daily Mail, yanaonyesha kuwa utafiti huo uliangalia uwezo wa watoto zaidi ya 5,000 katika Kusoma, Hisabati na Sayansi.
Watafiti hao kwa kuangalia alama za majaribio mbalimbali na maoni ya walimu, waligundua kuwa hata katika hatua za awali (chekechea), alama za watoto wa kike zimekuwa juu siku zote ikilinganishwa na alama za watoto wa kiume.
Mmoja wa watafiti hao, Christopher Cornwell, anasema kuwa ujuzi wa wanafunzi hao, ndiyo njia kubwa inayotumiwa na walimu kuwapanga wanafunzi wao katika madaraja.
Aliongeza kuwa kuna vigezo sita vya kupima uwezo wa watoto, ambavyo ni: Usikivu, ufuatiliaji wa kazi anazopewa darasani, kupenda kujifunza, kusoma kwa kujitegemea, uwezo wa kubadilika kutokana na mazingira na mpangilio wa mambo yake.
Soma  zaidi :  http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/-/1597296/1664388/-/11r2tvs/-/index.html
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top