Social Icons

Loading...

Kura ya maoni yampa ushindi Raila Odinga uchaguzi Kenya

WAZIRI Mkuu Raila Odinga na Makamu wa Rais, Kalonzo Musyoka wamepewa ushindi wa awali katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Machi 4 nchini Kenya.
Kwa mujibu wa kura ya maoni ya Infotrak, iwapo uchaguzi ungefanyika wiki hii, Odinga anayewania wadhifa wa kuongoza nchi hiyo kupitia muungano wa Cord angeshinda kwa asilimia 51 ya kura.
Raila ambaye ni Waziri Mkuu katika Serikali inayomaliza muda wake ndiye mgombea urais kupitia muungano huo, pamoja na mgombea mwenza, Musyoka ambaye ni makamu wa Rais katika Serikali hiyo.
       Kwa mujibu wa matokeo ya utafiti huo uliofanywa na kampuni ya Infotrak and Consulting, Raila na Kalonzo watapata asilimia 51 ya kura zote zitakazopigwa huku wapinzani wao wakuu, Uhuru Kenyatta na William Ruto wanaowania wadhifa huo kwa tiketi ya muungano wa Jubilee wakipata asilimia 39.
Hii ina maana kuwa iwapo mambo yakisalia yalivyo, uchaguzi wa urais hautaingia katika awamu ya pili.
       Kura hizo za maoni pia zinaonyesha mgombea urais wa Muungano wa Amani, Naibu Waziri Mkuu,  Musalia Mudavadi na Muungano wa Eagle unaoshirikisha na Peter Kenneth na Raphael Tuju wanashika nafasi ya tatu kwa kuzoa asilimia 3 ya kura hizo.
Wagombea wengine wanaoshiriki katika uchaguzi huo wa urais kwa tiketi za vyama vyao bila kuungana na vyama vingine,
Martha Karua na Professa James Ole Kiyiapi wamepata asilimia 0.3 na 0.1.
Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo, Angela Ambitho alisema kuwa katika utafiti huo, watu 1,500 walihojiwa.
Alisema kura hiyo ilifanyika kabla ya Mudavadi kuteuliwa rasmi kama mgombea urais wa muungano wa Amani unaoshirikisha chama chake cha United Democratic Forum (UDF), Kanu na New Ford Kenya.
Utafiti huo ulifanyika kati ya Desemba 28 mwaka jana na Januari 2 mwaka huu katika kaunti 25 kwenye mikoa yote nchini.
Chanzo  Mwananchi
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top