SAKATA la gesi sasa limeingia hatua mpya, baada ya watendaji
wakuu wa CCM; Katibu Mkuu, Abdulrahman Kinana na Katibu wa Itikadi na
Uenezi, Nape Nnauye kuitaka Serikali ikae na wana-Mtwara ili kuona namna
ya kumaliza mgogoro huo kwa amani.Kinana na Nape walitoa kauli hizo kwa nyakati
tofauti jana. Wakati Kinana alisema hayo alipokuwa akizungumza katika
mkutano wa hadhara mkoani Kigoma, Nape alifanya hivyo kupitia mtandaowa
Twitter na baadaye kuthibitisha kauli hiyo alipoulizwa na mwandishi
wetu.
Wakati watendaji hao wa CCM wakitoa matamko hayo, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda jana alifanya vikao mfululizo mkoani Mtwara akisaka suluhu ya mgogoro huo.
Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Ofisi za CCM Wilaya ya Uvinza, Kigoma, Kinana aliitaka Serikali isikilize hoja za wakazi wa Mtwara na kuzitafutia usumbufu sahihi.Mbali na kutoa ushauri huo, aliitaka pia Serikali kuwasaka watu wanaochochea mgogoro huo kwa kufanya vurugu na kuharibu mali za watu na kuwafikisha mbele ya sheria.
“Serikali ikae na wana-Mtwara na kuwasikiliza, wananchi hao wana hoja na Serikali inapaswa kutoa majibu sahihi kwa hoja hizo. Lakini pia iwasake na kuwachukulia hatua za kisheria waliosababisha uvunjifu wa amani,” alisema Kinana.
Soma zaidi : http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/-/1597296/1678154/-/11rr4f4/-/index.html
Post a Comment