Social Icons

Loading...

Kutoka mtaji wa Sh2 milioni, mpaka Sh4 bilioni kwa mwaka.

Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba (wa tatu kulia), akimkabidhi tuzo Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Helvetic Solar Contractors, Patrick Ngowi (kulia) baada ya kuibuka mshindi wa kwanza mwaka 2012 wa Kampuni 100 Bora za Kati nchini (Top 100 Mid- Sized Companies).  Kushoto ni Mkurugezi wa Ufundi , Ephraim Kimati na Dada wa mshindi wa tuzo hiyo, Irene Ngowi.
Mafanikio ya biashara hayaji kwa usiku mmoja (overnight), lakini ukiwa na nia ya kufanikiwa, siku moja ndoto zako zitatimia.Mhandisi Patrick Ngowi, anaweza kuwa kati ya wafanyabiashara wachache nchini ambao ndoto zao za kuwa wafanyabiashara wakubwa, zimetimia angali wakiwa bado vijana wadogo.Ngowi ambaye wazazi wake ni walimu wa shule za sekondari, alianza safari yake ya biashara baada ya kumaliza kidato cha sita katika Shule ya Sekondari ya Azania jijini Dar es Salaam wakati huo akiwa na miaka 19.Anasema kuwa baada ya kumaliza kidato cha sita alihitajika kukaa nyumbani mwaka mmoja wakati akisubiri matokeo ili kwenda chuo kikuu.“Sikupenda kukaa nyumbani bila kufanya kitu chochote, nilitamani kufanya kitu chochote kitakachoniweka bize,” anasema. 
Mama alinikopesha mtaji wa Sh2.3.
Anasema mama yake, Emmy, alimkopesha Sh2.3 milioni, lakini sasa Kampuni yake ya Helvetic Solar Contractors sasa inaingiza mapato ya Sh4 bilioni kwa mwaka.
Baada ya kupata fedha hizo, anasema rafiki yake mwingine ambaye kwake ni sawa na kaka, alimpa tiketi ya ndege pamoja nyaraka zote na kusafiri mpaka China ambako alinunua simu kuja kuziuza Tanzania.

“Biashara ile ilikuwa na faida, sisi tulikuwa tunanunua simu moja kwa dola mbili za Marekani tunakuja kuuza Dola 18.“Mwanzo kabisa nilikuwa na wazo tu na tiketi ya kwenda China,  baada ya kutembelea China, niliamua kutafuta fedha kwa ajili ya kufanya biashara ya kuuza simu za mkononi, kutokana na faida niliyopata  baadaye nilikuwa na uwezo kufungua kampuni.“Msingi wa yote haya ni mama yangu pamoja na na muungwana mwingine waliokubali kunipa mkopo ambao haukuwa na riba,” anasema.Ni wazi kuwa, baada ya Ngowi kuona biashara ya simu haitamsaidia kufikia ndoto zake, aliamua kusoma masomo ya umeme wa jua katika Chuo Kikuu cha Dezhou  mchini China.

Lakini pamoja na hayo Kampuni ya Ngowi,  Helvetic Solar Contractors, mwaka huu imeshika namba moja kati ya kampuni bora 100 za kati zinazokua kwa kasi (Top 100 Mid-sized Companies 2012). Wakati Ngowi akisoma alikuwa akiendelea  na biashara ya kuuza simu.Mgao wa umeme wampatia mabilioniKwa mujibu wa taarifa za Serikali, kati ya zaidi ya Watanzania milioni 40, asilimia 14 pekee ndio wanaotumia umeme wa gridi ya taifa.
Kutokana kuliona hilo, kabla ya kuhitimu masomo yake, aliamua kusajili kampuni yake ya  Helvetic Solar Contractors.Mwaka 2008 akiwa na miaka 23, alirejea nchini akiwa mhitimu katika fani ya masuala ya umeme wa jua huku akiwa tayari amesajili kampuni yake.
Pamoja na kuwa na akiba aliyoweka kutokana na mauzo ya simu, bado alihitaji mtaji zaidi ili aweze kufanya biashara hiyo ya kuagiza na kufunga sola.Wakati akifikiri hilo, alipata rafiki mwingine ambaye ni Raia wa Uswiss, Philippe Glauser ambaye alikubali kumkopesha kiasi cha fedha bila riba.
“Hivyo ndivyo kampuni ilivyoanza, wakati huo ikiwa haina hata gari na mimi nikiwa mwenyewe, kwa mwaka wa kwanza niliweza kutengeza faifa ya Sh30 milioni,” anasema.
Hivi sasa anasema kampuni yake ina magari 14, Land cruiser saba, pickup tatu, Magari mawili ya madogo (salon) na  VX mbili.Pia anasema  kampuni hiyo kwa sasa ina wafanyakazi 16, nane kati yao wakiwa wamesomea mambo ya umeme.Pamoja na kuwa na wazo pamoja na kufungua kampuni, anasema watu wengi kutokuwa na uelewa wa kutosha juu ya faida na matumizi ya nishati hiyo ilikuwa ni changamoto kwake alipokua akianza kazi.“Daima mwanzo ni ngumu.
 Mwaka 2007 siyo watu wengi walikuwa wanajua umuhimu wa  nishati ya jua au jinsi inavyoweza kutumika, mgao wa umeme wa mwaka 2011 ulifanya watu waanze kutafuta vyanzo vingine mbadala vya nishati na kwa wakati huu sisi pekee ndio tuliokuwa miongoni mwaka kampuni kubwa zilizoweza kutoa majibu ya tatizo hilo,” anasema.
Anasema baada ya kutimia mwanya huo wa mgao wa umeme, wamepata soko zaidi baada ya kutoa bidhaa bora, kwa wakati na vifaa vyao kuwa na dhamana ya muda mrefu kwa wateja. “Kwa sasa sisi ni kati ya kampuni maarufu za kutoa huduma hii Tanzania, pia tumechaguliwa kusambaza bidhaa hii katika nchi nyingine za Afrika Mashariki, tuna timu kusambaza na kufunga vifaa hivi,” anasema.

Anasema ili kuboresha huduma zao wanashirikiana na kampuni kutoka nchi za magharibi lengo likiwa ni kufanya vizuri sokoni.Ngowi anasema kampuni yake ilianza kwa kutumia vifaa kutoka China, lakini kwa sasa wana tumia vifaa Marekani, Ujerumani, hispania na Israeli.Ngowi kuwasomesha wafanyakazi wake Ujerumani.Anasema kwa kuwa mafanikio ya kampuni yanatokana na wafanyakazi wake, moja kati ya mambo wanayozingatia ni kuwaendeleza kielimu.Ngowi anasema,  wanafikiria kuwapeleka Ujerumani kwenye mafunzo ili wafikie viwango vya kimataifa.

Anasema mbali na ofisi ya Arusha waliloanza nayo mwaka 2007, sasa wamefungua ofisi  Moshi, Dar es Salaam na mwaka 2013 watafungua nyingine Mwanza.“Wito wangu kwa vijana, siku zote wajue kuwa  jambo la msingi ni kuwa na wazo la kile unachotaka kufanya, kuwa na mtaji bila wazo ni sawa na bure, kuwa na wazo kisha panga namna ya kulitekeleza,  baada ya hapo muombe Mungu atakuongoza,” anasema Ngowi.Pia anasema elimu ya ujasiriamali kwenye shule za msingi na sekondari ni moja ya vitu muhimu vinavyoweza kuwainua wajasiriamali nchini.

Source: http://www.mwananchi.co.tz/Makala/-/1597592/1598180/-/8troiq/-/index.html
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top