Social Icons

Loading...

STEVEN WAMBURA:Msanii wa muziki wa Injili aliyeamua kuwekeza kwenye studio.

Steven Wambura
 MUZIKI wa Injili umekuwa ukikua siku hadi siku na kuzidi kuibua vipaji miongoni mwa jamii hasa vijana.
Steven Wambura ni mmoja wa vijana hao ambapo sasa ni msanii wa muziki wa Injili, huku muziki wake ukiwa ni wa bolingo na rumba.Kipaji cha Wambura kilianza kuonekana mwaka 1987 alipokuwa akiimba kwaya katika Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG), Bethel Kijenge mkoani Arusha.
“Wakati huo nilikuwa bado nikisoma, na masomo yangu yalikuwa magumu, nakumbuka nilipigwa na wazazi na wakati mwingine kulazwa njaa kutokana na kujihusisha na masuala ya muziki,” anasema.
Wambura anasema kuwa kipindi hicho wazazi wake walikuwa hawapendi ajishughulishe na muziki na kwamba mara zote walikuwa wakimsisitizia asome.
“Siwezi kuwalaumu, inawezekana walikuwa wanaogopa kwa sababu kulikuwa na dhana kuwa muziki wa Tanzania haulipi, lakini sasa muziki ndiyo unaendesha maisha yangu,”anasema.
Anaeleza kwamba baada ya kumaliza kidato cha nne mwaka 1993, aliendelea kuimba kwaya hadi mwaka 1994, alipoamua kuanzisha bendi yake iliyoitwa Chipukizi, ambayo alidumu nayo hadi mwaka 1997.
“Bendi haikudumu sana na mwaka 1998 niliajiriwa kwenye duka moja la dawa mkoani Arusha. Mwaka uliofuata niliamua kwenda nje kutafuta maisha,” anasimulia.
Studio  ikizinduliwa  kwa  maombi  na  baadhi  ya  viongozi wa makanisa  Dar.
 Anasema kuwa mwaka 2003 alirudi nchini na kuendelea na shughuli za uimbaji, ambapo aliamua kutoka kwenye mfumo wa kwaya na kuwa muimbaji binafsi.
Wambura anaeleza kuwa wakati akiendelea na shughuli za uimbaji binafsi, aliamua kuokoka mwaka 2005 na Mungu kumjalia kutoa albamu mbili ambazo ni Bwana ndiye bwana na Roho wa bwana.
Baadhi ya nyimbo zilizomo kwenye albamu hizo ni Bwana ndiye bwana, Bwana ndiye mchungaji wangu,  Ita jina la yesu,  Upendo,  Nilitembea tembea, Bwana u sehemu yangu,  Usilie tena na Nataka nikujue.
Mchungaji Kiongozi  wa  kanisa la Kinondoni   Revival  Church (KRC) TAG    Askofu  Dr Rogathe Zakayo  Swai  akipiga  baadhi ya  vyombo  katika  studio  ya  Steven  Wambura .
 “Albamu zote hizi zilifanya vizuri sokoni na kunivutia niendelee na muziki,”anasema.
Hata hivyo, anasema kuwa licha ya mafanikio aliyoyapata katika uimbaji, alikuwa na ndoto ya kumiliki studio yake binafsi, ambayo itajikita katika uandaaji wa muziki, vipindi maalumu pamoja na mahubiri.
“Msukumo wa kuanzisha studio hii na kuwekeza kiasi kikubwa cha fedha lengo lake siyo kufanya biashara, bali kuujenga ufalme wa Mungu na kuwasaidia wengine kutimiza ndoto zao,”anasema Wambura.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top