Social Icons

Loading...

DPP amfutia kesi mshirika wa Ponda- ULINZI MKALI WATAWALA

MKURUGENZI wa Mashtaka nchini (DPP), amemfutia kesi mmoja wa washtakiwa waliojumuishwa katika kesi inayomkabili Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda na wenzake.Pia katika kesi hiyo iliyofunguliwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, hakimu ameuamuru upande wa mashtaka uache utaratibu wa kumwingiza mahakamani mshtakiwa wa kwanza, Sheikh Ponda akiwa amefungwa pingu.

Aliyefutiwa mashtaka jana ni mshitakiwa wa 35 katika kesi hiyo, Rashid Omar.Wakili wa Serikali Mwandamizi, Tumaini Kweka ndiye aliyetoa taarifa kuhusu uamuzi huo wa DPP wakati wa usikilizwaji wa maelezo ya awali wa kesi hiyo jana.
 Sheikh Ponda Issa Ponda akizungumza na wakili wake
                                            Watuhumiwa wakiwa mahakamani


   Askari  maalumu   wakiwa  tayari  kwa  varangati   lolote
                              Hapa   fanya  fujo  uone -  Jamaa  wana  kiu    kwelikweli  na  chafuko  lolote .
   Doria     kama  kawa
     Ulinzi   kama   dawa  vile ,  hapiti  mtu  pasiko  kukaguliwa
                                           Du   hadi   inatishaa ,   cheki  hapa...

  Ulinzi   kama  kawaida   ulikuwa  mkali  ,  ili  kudhitibi  usalama  wakati  wa  kesi  ikisomwa.
Picha    na  Taarifa  kwa  hisani  ya  gazeti  la  mwananchi  na    blog  ya   http://richard-mwaikenda.blogspot.com/
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top