Social Icons

Loading...

SuperSports Waanza 'Supa Wikiendi'

KITUO cha televisheni cha SuperSport cha Afrika Kusini kinatarajia kuonyesha mechi nane za watani wa jadi kutoka sehemu mbalimbali duniani mwezi Oktoba ikiwamo mechi ya Simba na Yanga.
Kati ya mechi hizo za watani wa jadi itakayoanza kuonyeshwa itakuwa ni mechi kati ya Simba na Yanga hapo Oktoba 3 kupitia chaneli ya SuperSport 9east.
Crew  ya  SuperSports iliyoko  Tanzania  wiki hii.

Meneja uhusiano wa MultiChoice Tanzania, Barbara Kambogi alisema hayo wakati alipotembelea ofisi za Mwananchi Tabata Relini jijini Dar es Salaam, mechi nyingine za watani wa jadi zitakazoonyeshwa na kituo cha SuperSport mwezi Oktoba ni kati ya Barcelona dhidi ya Real Madrid (Hispania), Boca Juniors dhidi ya River Plate (Argentina) na Borussia Dortmund dhidi ya Schalke (Ujerumani).
Mechi nyingine ni kati ya Ajax Amsterdam dhidi ya Feyenoord Rotterdam (Uholanzi), Liverpool dhidi ya Everton (England), Inter Milan dhidi ya AC Milan (Italia) na CSKA dhidi ya Spartak (Russia).
Pia Kambogi alisema kuanzia leo kituo cha SuperSport kitaanza kuonyesha baadhi ya mechi za Ligi Kuu ya Tanzania, ambapo leo itaonyeshwa mechi kati ya Azam dhidi ya JKT Ruvu kuanzia saa 11:45 jioni.
Mechi nyingine zitakazoonyeshwa na SuperSport ni kati ya Simba dhidi ya Tanzania Prisons kesho, Yanga dhidi ya African Lyon siku ya Jumapili, JKT Ruvu dhidi ya Mtibwa Sugar siku ya Jumatatu kabla siku ya Jumatano kuonyesha mechi ya Simba na Yanga.
Naye mchambuzi wa soka katika kituo cha SuperSport, Thomas Mhlambo raia wa Afrika Kusini aliyekuwa ameambatana na Kambogi alisema muda siyo mrefu Tanzania itakuwa na wachezaji wa soka wengi wanaocheza soka katika nchi mbalimbali ulimwenguni.
  Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga (kulia) akizungumza na watangazaji maarufu wa Kampuni ya Super Sport ya Afrika Kusini, Thomas Mlambo (kushoto) na Thomas Kwenaite wakati wa hafla ya uzinduzi wa kampuni hiyo kuanza kwa majaribio kutangaza baadhi ya michezo ya Ligi Kuu ya Vodacom nchini katika hafla iliyofanyika Dar es Salaam jana
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top