Social Icons

Loading...

Breaking Newsssss!!!!Vurugu Kubwa zatokea Tegeta

Kumekuwa na hali ya taharuki katika eneo la Tegeta, Namanga karibu na kituo cha Mafuta cha Big Bon jijini Dar es salaam baada ya wananchi wenye hasira kuanza kurushiana mawe na Mapanga na watu waliotumwa kubomoa Vibanda vilivyo katika eneo hilo.Katika tukio hilo watu Wawili wamejeruhiwa vibaya na wamekimbizwa katika Hospitali ya Mwananyamala kwa ajili ya matibabu zaidi.Kwa mujibu wa Kamanda KENYELA kikundi cha watu kilifika katika eneo hilo na kuanza kubomoa Vibanda vilivyo katika eneo hilo la Namanga hali iliyowashtua wananchi wa eneo hilo na kisha kuanza kurushiana Nawe na Mapanga na kikundi hicho cha watu.Hata hivyo watu Wawili wanashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa huo wa Kinondoni kwa mahojiano zaidi kama wana uhalalali wa kubomoa Vibanda hivyo na wametumwa na nani.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top