Social Icons

Loading...

TIDO AJIUNGA AZAM MEDIA.

Tido  Mhando
Kampuni ya Azam Media inayomiliki pia Kituo cha Azam TV, itaanzisha stesheni ya redio hadi kufikia Machi mwakani, pia imemteua Tido Mhando kuwa Naibu Mkurugenzi Mtendaji.
Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Uhai Production Ltd iliyo chini ya Azam Media, Tido Mhando alisema kuwa mpango uliopo sasa ni kuhakikisha matangazo ya televisheni na redio yanawafikia wananchi kwa weledi wa hali ya juu.
Akizungumzia uteuzi wake, Mhando alisema uteuzi huo umempa changamoto ya kufanya kazi kwa ufanisi ili kuifanya Azam Media kuwa kampuni bora katika utoaji wa habari na burudani ukanda wa Afrika.
“Ninayo furaha kubwa kujiunga na Azam Media, pia na changamoto kubwa zilizopo mbele yetu kuifanya kuwa kampuni pekee ya televisheni na redio yenye ubora katika kutoa burudani hapa nchini na ukanda wote wa Afrika,” alisema Mhando.
Mhando aliyewahi kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Mwananchi Communications Limited (MCL), alisema kwa sasa ujenzi wa studio za kisasa Afrika Mashariki na Kati unafanyika na utakapokamilika, itakuwa ya aina yake kwa Afrika Mashariki na Kati.
Akizungumzia uteuzi wa Mhando, Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Azam Media Ltd, Rhys Torrington alisema uteuzi huo umefanyika huku wakitarajia makubwa kutoka kwa nguli huyo wa tasnia ya habari katika kuipeleka mbali Azam Tv.
Tunayo faraja kubwa kwa Tido kujiunga nasi wakati tunakaribia kutimiza mwaka wetu wa kwanza tangu kuanza kutoa huduma na Azam Tv,” alisema Torrington.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top