Social Icons

Loading...

UTAFITI : WATANZANIA WENGI BADO TUNATUNZA FEDHA NYUMBANI .

Asilimia 70 ya Watanzania wanatunza fedha zao nyumbani badala ya mfumo rasmi ukiwamo benki na huduma nyingine za fedha, imebainika.
Hayo yamebainishwa kwenye ripoti ya FinScope iliyotolewa jana na Mfuko wa Kuendeleza Huduma za Fedha Tanzania (FSDT), ikionyesha kuwa benki nchini zimeongezeka na kufikia 50.

Utafiti huo uliohusisha watu 8,000 umeonyesha kuwa asilimia 70.4 ya Watanzania milioni 24.2 wanaostahili kupata huduma za fedha, hawazitumii kutokana na sababu mbalimbali.

Sababu hizo ni pamoja na ukosefu wa elimu ya masuala ya fedha, umbali kufikia matawi ya benki au wakala, gharama kubwa za uendeshaji wa huduma hizo, mazoea ya mfumo wa kijima wa utunzaji wa fedha, kukosa imani kuhusu usalama wa fedha zao.

Akizindua ripoti hiyo, Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Benno Ndulu alisema jana kuwa pamoja na hali hiyo, kumekuwa na maendeleo makubwa katika sekta hiyo ukilinganisha na hali ilivyokuwa miaka minne iliyopita.
Soma  zaidi  mwananchi .
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top