Social Icons

Loading...

Mimi siyo Rais, asema Lowassa .

Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowasa amewataka waendesha bodaboda na watu wengine wasimwite Rais kwa sababu wanamtengenezea chuki na uhusiano mbaya na watu.

“Mbona mnataka kuniletea uchuro! Mnanitengenezea ugomvi na watu jamani…,” alisema wakati akizindua Shirikisho la Bodaboda Tanzania jana kwenye Viwanja vya Leaders, Dar es Salaam.

Lowassa amekuwa akitajwa kuwania urais katika uchaguzi ujao wa Rais na wabunge utakofanyika 2015. Hatua hiyo imekuja baada ya Lowassa kuwaeleza kuwa atafanya harambee ya kuchangisha fedha ili kila aliyeingia kwenye shirikisho la waendesha bodaboda aweze kupata pikipiki yake.

Baada ya kauli hiyo waendesha bodaboda hao walipaza sauti zao wakiimba rais,rais …..wa mwaka 2015 huku wakidai amepita hana mshindani. Aliwataka kuacha  kumwita rais kwa sababu wanamtengenezea ugomvi na watu.

Alisema asilimia 50 ya madereva wanaoendesha  bodaboda hizo siyo pikipiki zao hivyo kutokana na hilo atafanya harambee ili kila mmoja kumiliki  pikipiki yake ili waweze kujiajiri wenyewe.

“Tumeona kuna tofauti kubwa kati ya matajiri na maskini hivyo nimeona kwenye shirikisho hili asilimia 50 siyo za kwenu.  Nimekusudia kuanzisha  harambee ya madereva ambao hawana pikipiki ili nao  wawe nazo waweze kujiajiri,” alisema Lowasa.

Lowasa aliitaka Kamati ya Shirikisho la Bodaboda kukutana naye Januari 15 mwaka 2014 ili kupanga harambee hiyo ifanyike lini na wapi.

Alisema matajiri nchini wapo wengi nitawafuata na kuwachangisha harambee wakiwemo Mwenyekiti wa Kampuni za IPP, Reginald Mengi na mfanyabiashara maarufu Said Salum Bakhresa.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top