Social Icons

Loading...

Mandela AIVUTA DUNIA S.A.



Viongozi zaidi ya sabini wakiwamo wakuu wa nchi na Serikali wanatarajiwa kushiriki hatua mbalimbali za safari ya mwisho ya Mzee Mandela aliyefariki Alhamisi ya Desemba tano usiku.

Anatarajiwa kuzikwa Jumapili ijayo, Desemba 15, 2013 katika Kijiji cha Qunu alikokulia, mazishi ambayo yanatarajiwa kuwavuta maelfu ya watu kutoka kona mbalimbali za dunia.
Hata hivyo hadi jana maofisa wa Serikali ya Afrika Kusini walisema walikuwa bado hawajapata orodha kamili ya viongozi wote watakaohudhuria, l pia wakashindwa kusema iwapo Rais Obama atakwenda Qunu au atashiriki katika hatua nyingine za awali za msiba huo kabla ya mazishi ya Jumapili.
Msemaji wa Ikulu ya Marekani, Jay Carney alinukuliwa akithibitisha kwamba Obama na mkewe Michele watashiriki katika msiba huo lakini hakuwa tayari kueleza suala hilo kwa undani. Habari zaidi zilizopatikana jana mjini Johanesburg zinasema Rais wa Brazil, Dilma Rousseff atakuwa miongoni mwa wageni mashuhuri watakaoshiriki.
Balozi wa Marekani nchini Afrika Kusini, anasema kuwa: “Rais Obama, amethibitisha kushiriki mazishi ya Madiba” (akirejea) jina maarufu la Mzee Mandela, taarifa ambayo ilitiliwa na nguvu na habari zilizoinukuu Ikulu ya Washington ikithibitisha ujio wa kiongozi huyo pamoja na watanguliza wake; George W. Bush na Bill Clinton.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top