Social Icons

Loading...

Rais Obama achelewesha uamuzi wa kuivamia Syria


Rais Barack Obama amechelewesha kutoa uamuzi wa kuivamia Syria kijeshi baada ya kuazimia kulipeleka suala hilo bungeni ili liidhinishwe.Obama amechukua hatua hiyo wakati huu ambapo shinikizo la kuishambulia Syria na kumwondoa madarakani Rais Bashar al-Assad likizidi kushika kasi, kwa kile kinachodaiwa kuwa amekuwa akitumia silaha za sumu dhidi ya raia.

Mchakato huo unaendelea huku Rais wa Urusi, Vladmir Putin akimuonya Obama na kusema uvamizi wa kijeshi wa Syria ni suala lisilokubalika.Tayari Kansela wa Ujerumani Angela Merkel amezishutumu Urusi na China kwa kushindwa kushirikiana na nchi za Magharibi kumaliza umwagaji damu nchini Syria na kuzilaumu kwa kudhoofisha jukumu la Umoja wa Mataifa.
Katika mahojiano na gazeti moja la Ujerumani yaliyochapishwa juzi,  Merkel alizishutumu Urusi na China kwa kutatiza juhudi za nchi za Magharibi za kuutatua mzozo wa Syria.
Nchi hizo mbili ambazo ni wanachama wa kudumu katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa walitumia kura yao ya turufu kupinga maazimio mara tatu kuihusu Syria tangu vita vizuke nchini humo zaidi ya miaka miwili iliyopita.
Urusi na China zinatarajiwa pia wakati huu kupinga azimio linaloungwa mkono na Marekani na Uingereza lililowasilishwa katika baraza hilo ambalo ndilo lenye mamlaka ya kuidhinisha hatua za kijeshi dhidi ya utawala wa Syria kutokana na  madai ya matumizi ya silaha za kemikali siku kumi zilizopita viungani mwa Mji Mkuu Damascus.
Chanzo  mwananchi
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top