Social Icons

Loading...

Rais Kikwete aongoza mazishi ya Askofu Kulola.

Rais Jakaya Kikwete ameongoza maelfu ya waombolezaji kumzika aliyekuwa Askofu Mkuu Moses Kulola wa Kanisa la Evangelist Assemblies of God Tanzania (EAGT). Kiongozi huyo alizikwa jana nje ya Kanisa la Calvary Bugando.Licha ya kuongoza mazishi hayo, Rais Kikwete pia alitoa ushuhuda kwamba licha ya kuwa muumini wa dini ya Kiislamu, Askofu Kulola wakati wa uhai wake mara kadhaa alikwenda Ikulu kumfanyia maombi.
Rais Kikwete katika salamu zake za rambirambi, alisema amekwenda kushiriki msiba huo kuungana na waombolezaji kutokana na kumfahamu Askofu Kulola ambaye alikuwa mtu wa watu.
“Tuzidi kuwaombea kwa Mungu, familia katika kipindi hiki kigumu, kwa jinsi nilivyomfahamu marehemu alikuwa mpenda watu, hakujali kabila wala hali zao, alijali utu na heshima hii ndiyo sababu na mimi alikuwa rafiki yangu,” alieleza Rais Kikwete.
Alibainisha kwamba licha ya kuwa Muislamu mara kadhaa Askofu huyo alifika kumwombea Ikulu na katika maombezi yake alisisitiza kuwa alikuwa akiwaombea Watanzania na nchi nzima kwa ujumla, hivyo aliwahimiza walio hai kumuenzi Askofu kwa vitendo.

author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top