Social Icons

Loading...

Dr. Ndalichako aichanachana Elimu ya Tanzania.

Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani Nchini (Necta), Dk Joyce Ndalichako amesema karatasi za majibu ambazo wamekuwa wakizipata kutoka kwa wanafunzi zinaonyesha kuwa, watoto wengi wanahudhuria shuleni lakini hakuna wanachojifunza.
Dk Ndalichako aliyasema hayo jana jijini hapa alipokuwa akizungumza kwenye mkutano wa mabaraza ya mitihani ya Afrika, ambao umejikita kujadili suala la tathimini ya elimu kwa nchi za Afrika.
Hii ni mara ya kwanza kwa Dk Ndalichako kuzungumza tangu Serikali itangaze kufuta matokeo ya kidato cha nne mwaka 2012 na kutaka yapangwe upya, suala ambalo lilipingwa na wadau wengi wa elimu.
Alisema kuwa wakati nchi nyingi za bara hili zikiwa zimejitahidi kuongeza upatikanaji wa elimu kwa watu, ubora wa elimu unaendelea kuwa tishio kwa watu wa bara hili kwa vizazi vijavyo.“Kama mabaraza ya mitihani, tumekuwa tukiona karatasi za majibu kutoka kwa wanafunzi ambazo zinaonyesha kwa uwazi kabisa kuwa watoto wanahudhuria shuleni lakini hakuna wanachojifunza,” alisema Dk Ndalichako.
Chanzo   gazeti  la mwananchi
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top