Social Icons

Loading...

Tiper yaipa Serikali gawio Sh1 bil

Kampuni  ya Kuhifadhi Mafuta ya Tanzania International Petroleum Reserves Limited (Tiper), imekabidhi hundi ya Sh1 bilioni kwa Waziri ya Fedha, Dk William Mgimwa, ikiwa ni kama gawio la Serikali mwaka unaoishia  Desemba 31, 2012.Kampuni hiyo inamilikiwa kwa pamoja kati ya Serikali yenye hisa asilimia 50  na Kampuni ya Uswisi ya Oryx Oil and Gas (OOG) yenye idadi hiyohiyo ya hisa.
Akikabidhi hundi hiyo kwa Dk Mgimwa jana, Mkurugenzi Mtendaji wa Tiper, Daniel Belair, alisema gawio hilo litakuwa chachu ya maendeleo ya uchumi nchini.“Tunayo furaha kukabidhi hundi hii yenye thamani ya Sh1 bilioni,  ikiwa ni wajibu wetu kisheria kama kampuni. Tunaamini mchango wetu utasaidia kuchochea uchumi wa taifa,” alisema Belair.Alisema Tiper inatarajia kuongeza zaidi uwezo wa kuhifadhi mafuta na kufikia zaidi ya lita za ujazo 290,000 ifikapo mwaka 2015,  baada ya uwekezaji Dola 12 bilioni za Marekani.Belair alisema hivi sasa Tiper ina kituo kikubwa cha kuhifadhi mafuta nchini,  chenye uwezo wa kuhifadhi zaidi ya lita za ujazo 141,000 ikilenga kufikia lita za ujazo 215,000.“Katika uwekezaji mpya, tangi mbili zenye uwezo wa kuhifadhi lita za ujazo 36,600 zimeshaongezwa katika robo ya kwanza ya 2013,” alisema Belair na kuongeza:“Kipaumbele chetu kikubwa ni kuhakikisha kuwa bidhaa za mafuta ya petroli zinapatikana katika soko muda wote.”
Chanzo    mwananchi
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top