Rais Barack Obama wa Marekani aliwasili Dar es Salaam jana mchana
ikiwa ni nchi ya mwisho katika ziara yake barani Afrika ikitanguliwa na
Senegal na Afrika Kusini.
Akizungumza na waandishi wa habari pamoja na Rais
Jakaya Kikwete Ikulu, Rais Obama alisema aliainisha mambo hayo wakati
alipozungumza na mwenyeji wake huyo.
Alisema katika mazungumzo hayo, waligusia mradi wa
mkubwa wa umeme uitwao Power Afrika wenye lengo la kuongeza kiwango cha
umeme kinachozalishwa nchini na barani Afrika ili kupata umeme nafuu na
wa uhakika utakaochagiza kuongeza uzalishaji na kukuza ajira.Nchi nyingine za Afrika ambazo zitanufaika na mpango huo ni Kenya, Ghana, Liberia, Nigeria na Ethiopia.Rais Obama alisema pia wamezungumzia masuala
mbalimbali ya maendeleo, ukuzaji wa demokrasia na utawala bora.
Alimzungumzia pia mchezaji nyota wa mpira wa kikapu wa Tanzania, Hashimu
Thabeet anayecheza katika Ligi Kuu ya Marekani (NBA), akiwa na timu ya
Oklahoma Thunder ya Marekani, akisema hawakuzungumzia suala lake na
kuahidi kufanya hivyo siku nyingine.Akijibu swali iwapo anaridhishwa na misaada ambayo
nchi yake inatoa kwa Tanzania, Rais Obama alisema anafarijika kwa
matunda yanayopatikana katika mapambano dhidi ya malaria, barabara mpya
zinazojengwa na katika maeneo mbalimbali ya nchi.“Hatutoi dawa, bali tunajenga miundombinu ya afya,
hatutoi chakula, bali kuwezesha nchi kujitosheleza kwa chakula pia
tunasisitiza kubadilishwa kwa sheria mbalimbali ili kutoa fursa kwa
sekta binafsi kuleta mitaji yao kwa wingi zaidi, lakini jambo la muhimu
ni kuijenga Afrika,” alisema.
Post a Comment