Social Icons

Loading...

Qatar, Fly540 zakubaliana kushirikiana.

Kampuni ya Ndege ya Fly540 imesaini makubaliano na Shirika la Ndege la Qatar Airways, yenye lengo la kuwezesha abiria wa Qatar Airways kuendelea na safari za ndani na kanda kwa kutumia ndege za Fly540.
Chini ya makubaliano hayo, abiria wa Qatar Airways baada ya kufika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta, Kenya, wataendelea na safari zao mbalimbali kwa kutumia ndege za Fly540.
Shirika hilo la Ndege la Qatar huruka mara mbili kwa siku kwenye safari ya Nairobi-Doha, wasafiri wanaweza kuunga safari nyingine katika miji mikubwa barani Ulaya, Mashariki ya Kati na Asia Pacific.
Qatar Airways ilisema uamuzi wake wa kuchagua Fly540 kuwa kama mbia, unadhihirisha dhamira ya shirika hilo lenye makazi yake Doha kufanya uwekezaji eneo la Afrika Mashariki.
Msemaji wa Shirika la Fly540 la Kenya, alisema makubaliano hayo yanadhirisha jinsi shirika hilo linavyoaminika na kuhudumia mashirika makubwa kama la Qatar Airways.
“Tunayo furaha kufikia makubaliano haya na Shirika la Ndege la Qatar, ambayo ni makubaliano yetu ya kwanza ya pekee,” alisema Ofisa Mtendaji Mkuu wa Fly540 Kenya, Don Smith. Safari hizo zinahusisha Zanzibar, Juba na vivutio vya utalii.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top