KATIKA hali ya kawaida, tumezoea kuona watalii kutoka mataifa
mbalimbali duniani wakija nchini kuangalia vivutio vya utalii vilivyopo.Baadhi ya vivutio hivi ni Mlima Kilimanjaro, mbuga za wanyama, majengo ya kale, mapango na nyumba za kihistoria.Hata hivyo, kumeibuka aina mpya ya utalii,
unaojulikana kama utalii wa ngono, ambao unashamiri kwa kasi ukihusisha
zaidi watalii wanawake wanaofuata wanaume wa Kitanzania hasa vijana.
Uchunguzi uliofanywa na Mwananchi Jumapili,
unaonyesha kuwa utalii huo unaongezeka kwa kasi hasa katika maeneo yenye
vivutio vingi vya utalii ikiwamo Arusha, Kilimanjaro na Zanzibar.
Imebainika kuwa katika utalii huu, wanawake hasa
watu wazima walio na umri kati ya miaka 60 hadi 80 kutoka nchi
mbalimbali, wamekuwa wakiingia nchini kwa lengo la kutafuta vijana wa
kiume wa kustarehe nao.Uchunguzi huo unaonyesha kuwa wanawake ambao
hawana vigezo vya uzuri vinavyopendwa na wanaume huko kwao, ikiwamo
wembamba na urefu, husafiri kuja Tanzania kutafuta mwanamume
atakayestarehe naye kingono.Hali hiyo inawakumba zaidi wanawake wanene, ambao
kwa Ulaya hukosa wapenzi, hivyo kulazimika kusafiri kuja Afrika Tanzania
ikiwamo kutafuta mwenza wa kustarehe nao.
Chanzo: http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/-/1597296/1689836/-/11sei33/-/index.html
Chanzo: http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/-/1597296/1689836/-/11sei33/-/index.html
Post a Comment