Social Icons

Loading...

Rais wa TFF amewataka wadau wa soka kuwa katika hali ya utulivu.

  Rais wa shirikisho la soka nchini TFF Leodger Chilla Tenga 
 =====

Rais wa shirikisho la soka nchini TFF Leodger Chilla Tenga amewataka wadau wa soka kuwa katika hali ya utulivu, katika kipindi hiki cha kuusubiri ujumbe wa shirikisho la soka duniani ambao utakuja nchini mwezi ujao kwa ajili ya kutatua sakata la uchaguzi wa TFF.

Tenga ametoa rai hiyo kwa wadau, baada ya hali ya utulivu wa soka kuingia dosari kufuatia kila mtu kusema lake baada ya kamati ya rufa ya uchaguzi inayoongozwa na Iddi Mtiginjola kuliengua jina la aliekua mgombea wa nafasi wa uraisi wa TFF Malali Malizi kwa kigezo cha kukosa sifa za kugombea.

Hata hivyo Tenga ametoa msisitizo kwa wadau wa soka nchini kutambua kwamba sakata la uchaguzi wa TFF katu halitochukua mustakabali wa maandalizi ya mchezo wa kuwani nafasi ya kucheza fainali za kombe la dunia ambapo timu ya taifa Taifa Stars itapambana na timu ya taifa ya Morocco mwezi ujao.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top