Social Icons

Loading...

John Mnyika: Sheria mpya zinawalinda mafisadi.

MBUNGE wa Ubungo Jijini Dar es Salaam (Chadema), John Mnyika amemtaka, Rais Jakaya Kikwete kutosaini marekebisho ya sheria mpya ya mabadiliko katika Sheria ya Ukaguzi wa Hesabu za Umma ya 2008.Mnyika pia anakusudia kukata rufaa juu ya uamuzi wa Spika wa Bunge, Anne Makinda kwa kutumia vibaya kanuni za Bunge kutokana na kitendo chake cha kuzivunja kamati tatu za Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC), Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) na Hesabu za Serikali Kuu (PAC).
 Akizungumza na Mwananchi Jumapili, jana, Mnyika alisema Rais Kikwete kabla ya kusaini marekebisho hayo ambayo yanaonyesha dalili za kuwalinda mafisadi, ajitokeze na kuwaeleza Watanzania faida na hasara ya mabadiliko ya sheria hiyo.
       Wiki hii Serikali iliwasilisha bungeni mapendekezo ya mabadiliko katika Sheria ya Ukaguzi wa Hesabu za Umma ya 2008, huku ikiongeza vifungu ambavyo vinapunguza nguvu ya Bunge katika kushughulikia taarifa ya Ofisi ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).
Soma  zaidi  : http://www.mwananchi.co.tz/habari/-/1597578/1689870/-/vlipm8/-/index.html
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top