Social Icons

Loading...

Chadema yajipanga kwenda Ikulu 2015

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeanza mkakati wa kuhakikisha kinashinda Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2015 ili kukiwezesha kuingia Ikulu.
Kimesema kitatekeleza hatua hiyo pia kwa kufanya uchaguzi wa kuwapata viongozi wake wapya akiwamo mwenyekiti wa taifa, uchaguzi utakaofanyika ndani ya mwaka huu. Hata hivyo, tarehe, mwezi na ratiba kamili ya uchaguzi huo itatolewa baadaye.Kujipanga kwa chama hicho sambamba na kujenga hoja kulithibitika pia katika Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), mwaka jana mkoani Dodoma, baada ya mwenyekiti wake Rais Jakaya Kikwete kuwataka mawaziri na makada wa chama hicho kufanya mikutano ya hadhara na kutumia vyombo vya habari kujibu hoja za wapinzani, badala ya kutegemea nguvu za Jeshi la Polisi.Katika mkutano huo, Rais Kikwete alimtaja wazi Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk  Willibrod Slaa, akidai kuwa aliwahi kumzulia uongo pamoja na mwanaye Ridhiwani.Rais Kikwete alisisitiza kuwa hiyo ndiyo kazi ya upinzani, akiwaita watu wazima ovyo na kudai kwamba wanasema uongo mbele ya wananchi na kwamba hata wakati mwingine hunukuu takwimu za uzushi kwenye vyombo vya habari.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top