Social Icons

Loading...

Aomba asichaguliwe asipotimiza ahadi.


MBUNGE wa Jimbo la Iringa ,Mchungaji Peter Msigwa amewataka wakazi wa Kijiji cha Kigonzile, katika Manispaa ya Iringa kutomchagua katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 ikiwa hatatimiza ahadi ya kuwapelekea maji na barabara katika kipindi hiki cha uongozi wake.
Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Shule ya Msingi Kigonzile juzi, Msigwa alisema amepania kuwafikishia maji na barabara wakazi wa kijiji hicho ili kuwapunguzia kero ya kutafuta maji na adha ya usafiri.

“Ninajua kero ya maji na barabara ndizo zinazowatesa wakazi wa kijiji hiki hususani wakina mama, lakini niseme tu kwamba suala la maji, nimefurahi kuna mfuko mnaendelea kuuchangia deni lililobaki ninalimalizia sasa na kuhusu barabara tayari nimeshaleta greda nitahakikisha barabara hii inatengenezwa, nisipotimiza ahadi hizi msinipigie kura mwaka 2015,”alisema Msigwa.
Soma  zaidi :  http://www.mwananchi.co.tz/habari/-/1597578/1662934/-/vk5saf/-/index.html
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top