Social Icons

Loading...

Chagua Maisha Unayotaka Kuyaishi Na Uyaishi Kweli.

Na   Meshaki   Maganga  toka  IRINGA:
Wiki ya jana imekuwa wiki ya kazi nyingi na pilika za hapa na pale. Wiki hii nimebahatika kukutana na rafiki zangu ambao kwa muda mrefu tumekuwa tukiwasiliana kupitia mitandao ya kijamii na blog bila kuonana, kuna mmoja ambae aliamua kufunga safari kutoka Dar es slaam  mpaka Iringa kuja kujifunza uwekazaji kwenye mashamba ya miti na mboga mboga. Na ameamua kuwekeza kwa kununua ekari kumi za kupanda miti. Wiki hii nimejifunza kwamba, kila mtu ana uwezo wa kuchagua kufanya  yale ayatakayo  maishani, Dunia ina mengi ya kuyafanya na kuna kila nafasi kwa mwanadamu yeyote anayechagua kuwa anavyotaka maishani. Chagua maisha unayotaka kuyaishi na uyaishi kweli. 
Usiogope kujaribu kitu, maisha ya kuogopa kufanya kitu ni maisha yasiyo na maana. Usikubali maisha ya ‘ukawaida’ na ambayo yatakufanya usiishi maisha makubwa unayostahili.
Siri kubwa ya watu wenye mafanikio duniani, ni kuwa hawaogopi maisha, wapo tayari kuumia kwa kuchagua maisha wayatakayo.  Chagua kipengele mojawapo cha kijasiriamali  unachotaka kukifanya na ukifanye kweli kwa moyo wote. Jiendeleze kila siku katika ulilochagua kiasi ambacho utavunja mipaka na kuweka rekodi yako. Chagua kufanikiwa.
Wewe kama binadamu na sisi wengine wote, tuna mawazo ya aina moja tu hatuna aina zaidi ya moja. Lakini haya mawazo yetu yana sifa au tabia kuu mbili. Sifa hizi mbili zinatofautiana kabisa kana kwamba hazihusu kitu hichohicho.
Sifa hizi zimepewa majina mbalimbali tangu kufanyika kwa ugunduzi wake miaka maelfu iliyopita. Majina kama mawazo ya kawaida nay a kina, mawazo yaliyo machona yaliyolala, mawazo ya nje na ndani, mawazo yenye utashi na yasiyo na utashi, mawazo ya kike nay a kiume, mawazo razini na yasio –razini na majina mengine.Lakini katika makala hii   nitatumia maneno istilahi hizi- ‘mawazo ya kawaida na mawazo ya kina’ katika kuzungumzia jambo hili.
Ili tuweze kuelewa vizuri kuhusu tofauti ya sifa hizi mbili za mawazo yetu ni vizuri nitatoa  mfano hapa:- Tuchukulie mawazo yako kama bustani ni kile unachokifikiria  (fikra) kama mbegu ambazo unazipanda kwenye bustani hiyo. Kwenye mawazo yako ya kina, ndipo mahali ambapo mbegu hizo zinapopandwa, yaani zitakapoota. Baadae mbegu (fikra) hazaliwa kwenye miili na mazingira yanayotuzunguka.
Tunapofikiria jambo lolote. Fikira hizo huwa ziko kwenye mawazo yetu ya kawaida. Baada ya kuamini juu ya kile tunachokifikiri, ndipo ambapo fikira hizo huhifadhiwa kwenye mawazo yetu ya kina.
Wakati mwingine napengine mara nyingi huwa hatuna habari kwamba kile tunachokiamini kimehifadhiwa kwenye mawazo ya kina. Lakini kuhifadhiwa huku ni tofauti na kuhifadhiwa kwa maana ya kawaida tunayoijua. Mawazo ya kina yanapohifadhi fikira zetu huwa yanazifanyia kazi kwa kadiri zilivyokuja. Kama ambavyo tumeona kwenye mifano yetu ya awali kabisa ya mada hii, ni kile ambacho kinaombwa na mawazo  ya kawaida.
Tunaposema kile ambacho kinaombwa na mawazo  ya kawaida, tuna maana ya imani zetu, kile au yale yote tunayoyaamini. Kanuni ya ufanyaji kazi wa mawazo yetu ya kina ni imani zetu. Hakuna mtu anayeweza kuvunja kanuni hii kwani ni ya kimaumbile. Kwa hiyo, tunachokatikwa kukifahamu ni maana ya imani, kwa nini inafanya kazi na kwa namna gani.
Uzoefu wetu maishani, matukio, hali zetu za hisia na matendo yetu, vyote ni majibu ya mawazo yetu ya kina kwa mawazo yetu ya kawaida. Siyo kweli kwamba ni kile kitu au jambo tunaloliamini ndilo lene kupelekea matokeo Fulani kwenye maisha yetu, bali imani yetu kuhusu kitu au jambo hilo. Unapoamini katika ushirikina au hofu,  matokeo yake yatakuwa ni kulogwa, kuugua, hofu na kukata tamaa, lakini chenye kupelekea  hali hizo siyo ushirikina au hofu, bali inini yako kwenye hofu.
Mawazo yetu ya kina yakilishwa imani nzuri, yaani vitu au mambo mazuri, nayo hujibu vitu au mambo mazuri na yakilishwa imani mbaya nayo huzaa vitu au mambo mabaya. Mawazo haya huwa hayajui kuchuja au tunaweza kusema hayana “akili” kwani hayachambui kama imani iliyofikishwa kwake ni mbaya au nzuri, kwani zote huzifanyia kazi kwa namna moja, yakitaka kufanikisha kile ambacho kimeaminiwa na mawazo ya kawaida.
Watu ambao wana uwezo wa utumia vizuri mawazo yao ya kina wamefanikiwa sana maishani. Siyo kufanikiwa kwa mali bali zaidi kwa kuwa na furaha au vyote viwili. Wamekuwa na furaha maishani kwa sababu fikira zao siku zote zimekuea ni nzuri na wamemudu kufuta fikira mbaya kwenye mawazo yao. Kwa kufikiri kwao vizuri, mawazo yao ya kina yameweza kuzaa uzuri – mafanikio na furaha.
Wataalamu wengi wanakubali sasa kwamba, mawazo ya kina ndiyo ambayo kwa kiasi kikubwa yanabainisha aina ya maisha yetu. Hapo kabla wanasayansi wengi walikuwa wagumu sana katika kuukubali ukweli huu, lakini hivi sasa hata madaktari wa taaluma ya utabibu wanakubaliana na jambo hili.
Nimesoma utafiti wa Dr. Joseph Murphy ambaye amefanya utafiti wa kutosha kuhusu nguvu ya mawazo yetu ya kina anayaelezea mawazo haya kama nguvu kubwa alionayo binadamu katika kumwezesha kuboresha maisha yake, ingawa kwa bahati mbaya binadamu wengi hatujui kwamba tuna nguvu hiyo.Unaweza kuyapa maisha yako nguvu zaidi, uwezo zaidi, mali zaidi, afya zaidi, furaha zaidi na raha ya ziada, kwa kujifunza namna ya kuwasiliana na kutumia nguvu iliyojificha kwenye mawazo yako ya kina’,anasema kwenye kitabu chake cha The power of Subconscious Mind’.
Nguvu hiyo utaiipata vipi?  nitaeleza kwa kifupi hapa chini na kwa msomaji atakaependa anaweza kuniandikia kupitia barua pepe yangu.
Kama ambavyo tumesema ni kwamba kile ambacho hututokea kwenye maisha yetu ni matokeo ya majibu ya mawazo  yetu ya kina kwa kile amacho mawazo yetu ya kawaida yamekiamini. Tunapofikiri kwa kuamini kwamba, tumeshindwa, tuna mkosi, tumelogwa au tumekwama, taarifa hizi huenda kwenye mawazo yetu ya kina na kama tulivyobainisha, mawazo haya huwa yanaifainyia kazi imani yetu bila kujali kama ina faida kwetu au hapana. Kwa hiyo, ni wazi yataanza kufanyia kazi imani hizo na matokeo yake yataanza kuonekana sawia au baadaye kidogo, kwa nguvu au kidogo kidogo. Lakini ni lazima matokeo yatapatikana tu.
Hebu jaribu kuwatazama na kuwachunguza wale watu wanaoaini kwamba wana mkosi au wale wanaoamini kwamba, hawawezi. Mara zote utagundua kwamba, watu hawa hawatokwi na ikosi au hawafanikiwi abadani. Mikosi au kutofanikiwa huko huwajia kwa njia ambayo huwashangaza hata wao wenyewe. Hii ni nguvu ya mawazo ya kina.
Tunapoamini kuwa tuna mikosi au hatuwezi, mawazo yetu ya kina kwa kufuatana na kanuni za kimaumbile hutengeneza mazingira  ya kutupatia mikosi au kushindwa huko kwani mawazo hayo hutoa majibu kufuatana na kile kinachoenda kwenye mawazo yetu ya kawaida, yaani kile tunachokiamini.
Hebu jaribu kuwatazama na kuwachunguza wale watu wote wanaoamini kwamba wanaweza na wanaoamimi kwamba watafanikiwa. Mara zote utagundua kwamba, hatima ya watu hawa ni kufanikiwa na kumudu. Kinachowezesha hilo siyo kingine bali mawazo yao ya kina ambayo yamepokea taarifa hiyo kutoka kwenye mawazo ya kawaida ya watu hao, yaani kwenye imani zao.
Tukitaka kufanikiwa au kuanguka kwenye maisha yetu ni uamuzi wetu wenyewe. Tukizijaza fikira zetu kwa mawazo mazuri, yenye kutia moyo, ya upendo na uwezo, ni kkweli tutamudu na kufanikiwa. Tukiyajaza kwa kukata tama, hofu, kushindwa na kujibeza, matokeo yake yatakuwa ni ya kutuumiza, kutuangusha na kutuvuruga kwa kila hali.
Ni Lazima tukubali kwamba, sisi wenyewe ndiyo waumbaji wa maisha yetu kwa njia tuchaguayo kwa kuamini kwetu. Tukiamini na kujiambia kwa njia ya kutuporomosha, ni Lazima tutapotomoka. Tukiamini na kujiambia kwa njiaya kutuinua, ni Lazima tutainuka.  
Nimalizie kwa kusema “Kama unafikiri vibaya,utapata matokeo mabaya.Kama unafikiri vizuri utapata matokeo mazuri.Hii ni kwa sababu,binadamu hutenda na kuhisi kile anachokifikiri, kwani kisicho mawazoni mwake hakiwezi kumgusa kamwe”. 

Chanzo:  http://www.mjengwablog.com/2012/12/chagua-maisha-unayotaka-kuyaishi-na.html
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top