Social Icons

Loading...

SIMANZI NA MASIKITIKO...ULALE KWA AMANI .


Msanii maarufu katika tasnia ya Maigizo na Uchekeshaji marehemu Hussein Ramadhani Mtioeti (27) almaarufu SHAROMILIONEA aliyefariki kwa ajali ya gari jijini kijijini maguzo, Muheza,Tanga amezikwa leo mchan kijijini kwao. Maziko ya msanii huyu chipukizi aliyeanza kujijengea jina katika tasnia ya sanaa nchini yalijaa mamia kama sio maelfu ya watu wa kada mbalimbali na wasanii lukuki.

Mama yake SharoMillionaire (mwenye blauzi nyeusi) akilia kwa uchungu kwani Sharomillionaire ndiye alikuwa mtoto pekee wa kiume katika familia ya Mzee Mtoity.
Bestisto wa marehemu Sharomilionea Mzee Majuto akiwa pamoja na wasanii wengine wakijongea makaburini



Waombolezaji wakiubeba mwili wa marehemu Sharomillionaire kuupeleka katika nyumba yake ya milele

Mwili wa msanii chipukizi Sharomilionea ukiwa ndani ya Jeneza
Waombolezaji wakiuweka mwili wa marehemu Hussein Mteity "Sharomilionea" katika  kaburi

                              
                           Mwili wa Sharomilionea ukiswaliwa kabla ya kuwekwa mavumbini katika nyumba yake ya milele

Hussein Mteity "Sharomilionaire" umetutoka ungali mdogo sana tena wakati ambao nyota yako imeanza kung'aa.

Umewaachia simanzi na majonzi makubwa wapenzi wako wa tasnia ya maigizo hasa vichekesho. Naamini hata Airtel  matajiri wako wamepata pigo kubwa sana. Twaamini haki zako zitatunzwa nafamilia yako itanufaika.
SHAROMILLIONAIRE TUTAKUKUMBUKA !





                          







author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top