Social Icons

Loading...

Serengeti Boys yapata ushindi mwembamba

TIMU ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17, Serengeti Boys   imeifunga  1-0 dhidi  ya   Kongo Brazzaville,  kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam katika mchezo wa kwanza wa Raundi ya Tatu na ya mwisho kuwania tiketi ya kucheza Fainali za vijana wa umri huo Afrika zitakazopigwa nchini Morocco mwakani. Kwa matokeo hayo, Serengeti sasa inahitaji hata sare yoyote katika mchezo wa marudiano wiki mbili zijazo mjini Brazzaville ili kukata tiketi ya Morocco mwakani.
Kwa ujumla Serengeti walipigana katika mchezo wa leo, kwani wapinzani wao walionekana kuwa bora na wenye uzoefu zaidi yao.

Bao hilo lilifungwa kwa shuti la mpira wa adhabu na beki Mudathir Yahya Abbas kutoka umbali wa mita 22 na mpira kabla ya kutinga nyavuni ulimbabatiza beki mmoja wa Kongo na kumpoteza njia kipa Ombandza Mpea Joe na kujaa nyavuni.

Tanzania; Peter Manyika Peter, Miza Kriston Abdallah, Mohamed Hussein Mohamed, Ismail Adam Gambo, Miraj Adam Suleiman, Mudathir Yahya Abbas, Mohamed Salum Haroub, Joseph Kimwaga Lubasha/Dickson Isaac Ambundo, Hussein Twaha Ibrahim, Suleiman Hamisi Bofu/Tumaini Baraka Mosha na Farid Mussa Shah.
Kongo Brazzaville; Ombandza Mpea Joe, Tmouele Ngampio, Mabiala Gharlevy, Okimbi Francis, Ondongo Boungena, Ibra Vinny/Issambey Lonvreve, Binguila Handy, Obassi Ngatsongo, Mohendiki Brel, Atoni Mavoungou na Biassadila Arei.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top