Kufuatia matukio ya Uvunjifu wa Amani unaofanywa na kikundi cha watu
wachache kwa mwamvuli wa "dini". Kanisa La Kiinjili la Kilutheri
Tanzania (KKKT) limetoa Waraka Elekezi Wa Wachungaji Wake Wote Tanzania
kuelekeza kuwa siku ya tarehe 28 October, 2012 ni siku ya Kufunga na
Kuomba kwa ajili ya Amani nchini Tanzania.
Kanisa la KKKT linakuwa kanisa la Kwanza Tanzania kupitisha siku ya Kikanisa la Kufunga na Kuomba kwa ajili ya Amani Ya Nchi ilivyo Sasa.
Blog hii ambayo imefanikiwa kuutia machoni waraka huo uliotumwa na Maaskofu Dayosisi zote KKKT Wakuu wa Vituo vya Kazi za Umoja, KKKT na nakala yake kutumwa Manaibu Katibu Mkuu,Wasaidizi wa Maaskofu, Dayosisi zote KK KT, Makatibu Wakuu Dayosisi zote kuwaelekeza kwamba tarehe 28 Octoba ni Siku ya Kufunga na Kuomba. Waraka huo umeelekeza "Kufuatia matukio ya kuchoma Makanisa yaliyotokea hivi karibuni,barua inawataarifu kuwa siku ya Jumapili tarehe28 Oktoba 2012 imepangwa kuwa siku maalum ya kuombea amani katika nchi yetu.Pamoja na mambo mengine yaliyokwishakupangwa kufanyika siku hiyo ( 28 Oktoba2012)' tafadhali sharika, mitaa na Vituo vya Kazi za Umoja vyote vya Kanisa letu vifanye maombi hayo"
Kanisa la KKKT inawataka Waumini wa Kanisa hilo kuendelea Kuhimizwa Kufunga na Kuomba Kwa Kadri Roho Wa Bwana atakavyowaongoza kuombea amani ya Tanzania.
Chanzo kwa hisani ya : http://samsasali.blogspot.com/2012/10/kanisa-la-kkkt-iimetangaza-tarehe-28.html
Kanisa la KKKT linakuwa kanisa la Kwanza Tanzania kupitisha siku ya Kikanisa la Kufunga na Kuomba kwa ajili ya Amani Ya Nchi ilivyo Sasa.
Blog hii ambayo imefanikiwa kuutia machoni waraka huo uliotumwa na Maaskofu Dayosisi zote KKKT Wakuu wa Vituo vya Kazi za Umoja, KKKT na nakala yake kutumwa Manaibu Katibu Mkuu,Wasaidizi wa Maaskofu, Dayosisi zote KK KT, Makatibu Wakuu Dayosisi zote kuwaelekeza kwamba tarehe 28 Octoba ni Siku ya Kufunga na Kuomba. Waraka huo umeelekeza "Kufuatia matukio ya kuchoma Makanisa yaliyotokea hivi karibuni,barua inawataarifu kuwa siku ya Jumapili tarehe28 Oktoba 2012 imepangwa kuwa siku maalum ya kuombea amani katika nchi yetu.Pamoja na mambo mengine yaliyokwishakupangwa kufanyika siku hiyo ( 28 Oktoba2012)' tafadhali sharika, mitaa na Vituo vya Kazi za Umoja vyote vya Kanisa letu vifanye maombi hayo"
Kanisa la KKKT inawataka Waumini wa Kanisa hilo kuendelea Kuhimizwa Kufunga na Kuomba Kwa Kadri Roho Wa Bwana atakavyowaongoza kuombea amani ya Tanzania.
Chanzo kwa hisani ya : http://samsasali.blogspot.com/2012/10/kanisa-la-kkkt-iimetangaza-tarehe-28.html
Post a Comment