Social Icons

Loading...

Yanga Yatetea Ubingwa wake wa Kombe la Kagame


Mgeni  rasmi Mh:  Said Mecky Sadick Mkuu  wa  mkoa  wa  Dar  es Salaam  akikabidhi kombe   kwa  nahodha  wa Yanga Nadir Haroub Canavaro
MICHUANO ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame imefikia tamati jana Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kwa klabu ya Yanga, kufanikiwa kutetea taji lao, baada ya kuifunga Azam FC mabao 2-0.
 Shukrani kwao Hamisi Kiiza Diego na Said Bahanuzi, wafungaji wa mabao hayo moja kila kipindi na sasa Yanga inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager, inaingia kwenye orodha ya mabingwa wa kihistoria wa michuano hiyo, kwa kutwaa taji hilo mara tano.
Yanga sasa imebakiza mara moja kufikisha idadi sawa na wapinzani wao wa jadi, Simba (1974, 1991, 1992, 1995, 1996 na 2002) kutwaa Kombe hilo, mara tano kwa sita. Yanga ilibeba taji hilo 1975, 1993, 1999, 2011 na 2012.
Kiiza alifunga bao lake, baada ya kuuwahi mpira aliokuwa anarudishiwa kipa Deo Munishi ‘Dida’ na beki Said Mourad na kumpiga chenga kipa huyo kisha kuusukuma mpira nyavuni.
Bahanuzi aliuwahi mpira mrefu uliopigwa na beki Oscar Joshua na kuwazidi ujanja mabeki wa Azam kabla ya kumtungua Dida.
 Mechi hiyo ilichezeshwa vema na refa Thierry Nkurunzinza kutoka Burundi, aliyekuwa akisaidiwa na Simba Honore wa Rwanda na Peter Sabatia wa Kenya.
Katika mchezo huo kikosi kilichoweka historia ya Kombe la tano la Kagame, Yanga SC kilikuwa; Ally Mustafa ‘Barthez’, Stefano Mwasyika, Oscar Joshua, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Kevin Yondan, Athumani Iddi ‘Chuji’, Rashid Gumbo/Juma Seif ‘Kijiko’, Haruna Niyonzoma, Said Bahanuzi, Hamisi Kiiza na David Luhende.
Azam FC; Deo Munishi ‘Dida’, Ibrahim Shikanda, Erasto Nyoni, Said Mourad, Aggrey Morris, Jabir Aziz, Kipre Tcheche/Mrisho Ngassa, Salum Abubakar, John Bocco ‘Adebayor’, Ibrahim Mwaipopo na Ramadhan Chombo ‘Redondo’. Benchi; Mwadini Ally, Samir Haji Nuhu, Joseph Owino, George Odhiambo, Mrisho Ngassa, Khamis Mcha ‘Vialli’ na Gaudence Mwaikimba.
Katika mchezo uliotangulia wa kusaka mshindi wa tatu, AS ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) iliifunga APR ya Rwanda mabao 2-1, mabao yake yakifungwa na Magola Mapanda dakika ya 18 na Mutombo Kazadi dakika ya 67, wakati la kufutia machozi la timu ya jeshi la Rwanda, lilifungwa na Jean Mugiraneza dakika ya 89.  

author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top