Social Icons

Loading...

Kilichoiponza Simba kwa KCCA

Presha, pupa za kocha Zradvok Logarusic pamoja na kujiamini kupita kiasi kwa wachezaji na kukosa mipango katika safu kiungo na ushambuliaji vilichangia kuiua Simba.
Simba ilikubali kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa KCCA ya Uganda katika fainali iliyopigwa kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar.

Katika mchezo huo kocha wa Simba Logarusic alionekana kuchanganyikiwa na kufanya mabadiliko ya wachezaji wawili katika dakika 30 za kipindi cha kwanza.

Mcrotia huyo alimtoa beki Haruna Shamte dakika ya 19 za mchezo na kumwingiza William Lucia na dakika 29, alimtoa Awadh Juma na kumwingiza Ramadhani Chombo.

Pamoja na ujanja wa kocha Loga kujaza viungo wengi ili kutawala mchezo huo bado Waganda hao walifanikiwa kuharibu mipango yote ya Simba kwa kucheza soka ya kasi.
Taarifa  zaidi: http://www.mwananchi.co.tz/Michezo/Kilichoiponza-Simba-kwa-KCCA/-/1597534/2146718/-/e5vaye/-/index.html
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top