Social Icons

Loading...

Logarusic ampa ulaji kocha Yanga

Mabingwa wa Tanzania Bara, Yanga wamemsainisha mkataba wa miezi sita kocha wa zamani wa Berekum Chelsea ya Ghana, Hans Van der Plujim.
Mholanzi huyo kiboko wa kocha mkuu wa Simba, Zdravko Logarusic, mwaka 2012 alikiingoza kikosi chake cha Berekum Chelsea kuitandika Ashanti Gold Field mabao 4-0 iliyokuwa ikifundishwa na Mcrotia huyo.Uongozi wa Yanga umempa mkataba wa miezi sita kocha huyo huku ukimpa nafasi ya kuongeza mwaka mmoja endapo matokeo yatakuwa mazuri katika mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara.
Kocha Plujim alisema amekuja kufanya kazi na siyo vinginevyo kwani ana uzoefu wa soka la Afrika.
Alisema kuwa amefundisha soka Ghana na Ethiopia na anajua mazingira ya timu za Afrika hivyo amekuja Tanzania kuleta changamoto mpya.
“Nimekuja kufanya kazi na si kitu kingine, najua Yanga ni timu kubwa, ila wachezaji wanatakiwa kufuata sheria na kuwa na nidhamu ya hali ya juu, ndani na nje ya uwanja,” alisema Plujim (65).
Alisema kuwa staili yake ya ufundishaji ni kushambulia muda wote na kuweka ulinzi mkali wa kuzuia kufungwa.
soma  zaidi http://www.mwananchi.co.tz/Michezo/Logarusic-ampa-ulaji-kocha-Yanga/-/1597534/2145488/-/cx05llz/-/index.html
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top