Social Icons

Loading...

Vodacom, MCL wazindua habari kwa simu.

Kampuni ya Vodacom Tanzania na Mwananchi Communications Limited (MCL), zimezindua mradi wa kufikisha habari za punde (Breaking News) kwa jamii, kuanzia leo.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi huo Dar es Salaam jana, Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom, Rene Meza alisema kwa kuanzia, wanatarajia wateja wasiopungua milioni kumi kujiunga na huduma hiyo.
“Mtumiaji mtandao wa Vodacom ataunganishwa na huduma hii kwa kupeleka ujumbe wenye neno Habari kwenda namba 15569, kwa gharama ya Sh150 kwa siku, tunafurahia hatua hii kwani tuna hakika itatuimarisha sokoni,” alisema Rene.Naye Mkurugenzi Mtendaji wa MCL, Tido Mhando alisema mradi huo umegharimu mwaka mmoja na nusu kuuandaa.Mhando alisema mradi huo ni wa kitaifa na kimataifa, lengo ni kuwawezesha kupata habari yoyote kubwa, duniani na kuirusha papohapo kwa atakayekuwa amejiunga nao.
Chanzo :  http://www.mwananchi.co.tz/Vodacom--MCL-wazindua-habari-kwa-simu/-/1597570/1878420/-/ryt889z/-/index.html
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top