Social Icons

Loading...

Darasa Huru.

Wakati mwingine tukubali kujitazama kwa macho ya wengine na tutofautishe hali hii na kupewa ushauri katika mambo mbalimbali ya maisha.
Ninataka kutofautisha kujitazama kwa macho ya watu wanaotuzunguka na kupewa ushauri na watu wanaotuzunguka. Ushauri unaweza kupewa na kila mtu. Kila mmoja atakupa mawazo yake kutokana na uwezo wake wa kufikiri. Ushauri unaweza kupewa baada ya kuuomba au kuna wengine mabingwa wa kutoa ushauri wa bure watakufuata kutokana na misukumo mbalimbali ndani yao. Huu unaweza kuupuza kwa kuwa si kila unachoambiwa ufanye ni sahihi. Wengine watakushauri kutokana na makuzi yao, imani zao, uwezo wa kufikiri n.k. Ukifika hapa inabidi tu ukumbuke hadithi ya Mbayuwayu.
Yupo atakayekufuata kukushauri ubadili mwenendo fulani kwa kuwa kwa mtazamo wake wewe umetoka ‘nje ya reli’, wapo marafiki watakushauri uachane na mpenzi wako kwa kuwa ni kicheche na wazazi wanaweza kukushauri uachane na rafiki fulani kwa kuwa si mwema.
Huo ni ushauri ambao ninaamini umeshawahi kupewa mpaka nyingine zikakuvunja mbavu, kwa  maana mtu anakushauri uache kitu ambacho mwenyewe unaamini bora ufe kuliko kukiacha hicho. Mfano ni pale mlokole anapomfuata kijana wa ‘dot com’ akimshauri aache kwenda disko na kuvaa mlegezo
Kujitazama kwa macho ya wengine ni tofauti kabisa na kushauriwa, hii ni taswira ambayo unaipata baada ya kusikia maneno kadhaa yakirudia masikioni mwako kutoka kwa watu wa karibu yanayokuhusu wewe.
Kuna maneno umeyasikia mara kadhaa yakizungumzwa juu yako, wakati mwingine si kwa kukuteta bali wapo waliokwambia usoni kwako kuwa uko hivi na vile.
Hayo maneno ndiyo hasa taswira yako kwa wingine ambayo kwa uwezo wa kawaida wa kibinadamu si rahisi kujua. Hapa ndipo linakuja suala la kujitazama kwa macho yaw engine.
Mara ngapi umeambiwa wewe ni mvivu, mwoga, mzembe, chakubimbi,hupendi kujifunza na mengine kadha wa kadha?
Binafsi tangu mdogo nilikuwa naambiwa kuwa mzembe na si mfuatiliaji wa mambo muhimu. Ninakumbuka wakati niko shule ya sekondari kila mtu alikuwa ananiambia kama ukiacha kucheza na kusoma utakuwa wa kwanza nchi nzima kwasababu nilikuwa na akili sana lakini sisomi wala kuandika notisi.
Nimeendelea hivyo hata kazini bosi wangu alikuwa  akinisifu kuwa ninaweza kazi lakini siweki bidii ya kutosha kwani nikifanya hivyo ninaweza kuwa ‘best of the best’ katika kizazi changu kwasababu uwezo ninao.
Ilifika wakati nikafungua masikio na kuyasikiliza macho ya wengine yananitazamaje, nikagundua udhaifu wangu kupitia wao. Ingawa kwa miaka mingi niliupuuzia mtazamo huo lakini haukuweza kubadilisha ukweli.
Ni mara ngapi wewe mwenzangu umeambiwa upungufu wako, je umeyakubali au unawanunia watu na kuwaona wanakuonea. Sikiliza sauti hizi kwa makini, zikijirudiarudia jua kuna ukweli ndani yake.
fualitilia  zaidi  : http://www.mwananchi.co.tz/Makala/Kuna-wakati-tujitazame-kwa-macho-ya-wengine/-/1597592/1869294/-/ievsba/-/index.html
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top