Social Icons

Loading...

NANI KUWA RAISI WA KENYA AWAMU YA NNE. .

Wakenya wanapiga kura katika uchaguzi mkuu    leo  kwa mara ya kwanza tangu kupitishwa katiba mpya hapo mwaka 2010, inayoingia katika mfumo wa serikali ya kugawanya madaraka. Kura ya mwaka huu inajumuisha wagombea 1,882 kwa nafasi za kuchaguliwa, wabunge 290, maseneta 47, magavana wa majimbo 47, wawakilishi wanawake wa majimbo 47, kata za uraia 1,450 na nafasi ya uraisi.
         Kuna wagombea wanane wa urais, lakini kwa mujibu wa mwenendo wa kampeni, ushindani mkubwa upo baina ya Raila Odinga (68) wa Muungano wa CORD na Uhuru Kenyatta (52) wa muungano wa Jubilee. Wagombea wengine wa urais ni Musalia Mudavadi (53) kupitia muungano uitwao Amani, Martha Karua kupitia muungano wa NARC, Peter Kenneth (48) wa muungano wa Eagle, Mohamed Abduba Dida (39) wa muungano wa Alliance For Real Change (ARK), Paul Muite (68) wa Safina na Profesa James ole Kiyiapi (52) kupitia Restore and Build Kenya.

author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top