Social Icons

Loading...

CCM YASHINDA UCHAGUZI JIMBO LA KALENGA

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimeibuka kidedea katika uchaguzi wa kumpata Mbunge wa jimbo la Kalenga, baada ya kuzoa kura kwa asilimia 79.4 dhidi ya wapinzani wao Chadema waliopata asilimia 20.1 na Chausta 0.51.
Kwa nafasi hiyo, Mgombea wa CCM Godfrey Mgimwa amekuwa Mbunge mpya akichukua nafasi ya Mbunge aliyefariki jimboni humo, Dr William Mgimwa.
Matokeo ya uchaguzi huo, yanatoa nafasi nyingine kwa CCM kuweka rekodi ya kushinda chaguzi ndogo za ubunge katika majimbo mbalimbali yaliyokuwa nyameachwa wazi.
Kwa mujibu wa matokeo hayo, CCM imeshinda kwa kura 22,943 dhidi ya kura 5,800 za Chadema huku chausta ikiambukia 143.

author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top