Social Icons

Loading...

WAZEE WA JANGWANI TISHIO; VODACOM WAMEBANAAA SASA WAMEACHIA

DAR YOUNG AFRICAN SPORTS CLUB
Baada ya baraza la wazee wa Yanga kuketi na kutoa msimamo na tambo zao kwamba wao kama Yanga kamwe hawawezi kuvaa nembo au jezi yenye doa lenye rangi nyekundu na hawaogopi kufungiwa au kushushwa daraja.
Tambo hizo zilichochewa pia na maombi ya uongozi wa mabingwa hao wa CECAFA kwa VODACOM kwamba ni heri watumie nembo kama ya mwaka jana yenye rangi nyeusi na sio nyekundu.
Baada ya kilio na tambo hizo sasa VODACOM wamekubali ombi hilo na leo wamekabidhi aina tatu ambazo Yanga wanatakiwa kuchagua moja ili waitumie kama nembo ya mdhamini VODACOM.

NEMBO MPYA ZA VODACOM - YANGA

Kibarua sasa ni cha Yanga kuchagua nembo waitakayo na lazima sasa walinganishe na rangi ya nembo yao.

CHANGAMOTO KWA VODACOM NA TFF:
- Je! Timu ingine kama Toto Africa, JKT Oljoro, Africa Lyons, Kagera/Mtibwa Sugar au Azam FC nao wakisema kuwa nembo yenye kidoti chekundu nayo hairandani na rangi zao je nembo hiyo itabadilishwa?
- Je! Suala hili kisheria lina maana gani kwani tunatambua kuwa nembo huwa zinasajiliwa na kupewa copyright sasa VODACOM watakuwa wanasajili nembo kulingana na matakwa ya kila timu kila msimu wa ligi kwani timu zingine zitashuka na nyingine kupanda?

author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top